• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

NGO's ZATAKIWA KUONGEZA UWAZI KATIKA MIRADI WANAYOITEKELEZA KWA JAMII HUSIKA

Posted on: September 14th, 2022


Na Elinipa Lupembe.

Mashirika yasiyo ya kiserikali 'NGOs', halmashauri ya Arusha, yametakiwa kuweka wazi miradi wanayoitekeleza kwa jamii katika maeneo husika, lengo likiwa ni kila mwananchi kufahamu miradi hiyo katika maeneo yao.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Arumeru ambaye ni Mwenyekiti ya Kamati ya Mashirika hayo, Mkuu wa Kitengo cha Sheria halmashauri ya Arusha, Monica Mwailolo  wakati akifungua kikao cha kuwasilisha taarifa za Mashirika, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri hiyo, amebainisha kuwa, Serikali imeweka taratibu ambazo mashirika yanapaswa kufuata ikiwemo usajili, uwazi na uwajibikaji katika kutekeleza miradi hiyo.

Amebainisha kuwa kila shirika linalofanya kazi katika eneo husika ni lazima wananchi wa eneo hilo wapate taarifa sahihi za shirika hilo, ikiwemo shughuli zinazofanywa na endapo kuna mradi unatekelezwa, shirika liweke wazi mradi huo na gharama zake pamoja na muda wa utekelezaji wa mradi huo.

"Wananchi wanatakiwa kuzifahamu huduma mnazozitoa katika maeneo yao, hivyo ni lazima kuwafahamisha miradi mnayoitekeleza kupitia mbao za matangazo kwenye ofisi za kata na vijiji, ikionyesha  muda wa kuanza mradi na kukamilika kwake ili wananchi wapate kutumia huduma mnazozitoa katika maeneo yao na si kufanya kwa siri". Amesisitiza Mwanasheria

Imeelezwa kuwa, mashirika yanapaswa kutambua, nafasi ya Msajili wa NGO's, utekelezaji wa miradi kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali, pamoja na kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo kwa kila robo ya mwaka yaani kila baada ya miezi mitatu ya mwaka wa fedha husika.

Adha Mwenyekiti huyo ameweka wazi kuwa, Serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa na njema inayofanywa na kashirika hayo ya kuwahudumia wananchi na jamii, kazi ambazo amekiri kuwa ni utekelezaji wa vipaumbele vya Serikali ya awamu ya sita.

Naye Mratibu Masajili wa Mashirika, halmashauri ya Arusha, Ahadi Mlai, amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za mashirika hayo lakini pia, ni kukumbushana wajibu wa mashirika hayo kwa serikali na jamii.

Hata hivyo, wawakilishi wa Mashirika hayo, licha ya kuishukuru Serikali kwa kuwapa fursa ya kushiriki katika kuihudumia jamii, wameupongeza uongozi wa halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na taasisi hizo, jambo ambalo linafanya mashirika hayo kutekeleza majukumu yao kwa wepesi.

Wameongeza kuwa, vikao vya kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi kwa kila robo ya mwaka, ni vya muhimu kwa kuwa vinawakutanisha wadau wa mashirika pamoja na kuwapa fursa ya  kubadilishana uzoefu na namna ya kutatua changamoto zinazowakabili sambamba na kuongeza uwazi na uwajibikaji kwa serikali na mashirika hayo.

"Tunampongeza mkurugenzi na watalamu wake, kwa kushirikiana nasi katika kutekeleza miradi yetu, kila tunapohitaji msaada tunaupata kwa wakati, na kwa kukutana kila robo ya mwaka kutaongeza tija na ufanisi katika kazi na zaidi kufikia malengo ya mashirika na ya Seikali kwa ujumla wake" Amebainisha Elia Mbanguka Mratibu wa shirika la Destiny Foundation

Naye Meneja wa shirika la Kids Care International - Tanzania, Glory Swai, amesema kuwa licha ya mafanikio makubwa ya Serikali na mashirika, bado kuna changamoto kubwa ya ukatili dhidi ya watoto, huku jamii ikiwa na hofu ya kutoa taarifa na ushirikiano wakati wa kesi za ukatili, inayotokana na mila na desturi za kabila la kimaasai.

Awali Halmsahuri ina mashirika 42 yanayofanyakazi za kuhudumia jamiii, sekta ya elimu, afya, kilimo, haki za watoto, wanawake na vijana katika  maendeleo na Ustawi wa jamii.



Mkuu wa Kitengo cha Sheria halmashauri ya Arusha, Monica Mwailolo  wakati akifungua kikao cha kuwasilisha taarifa za Mashirika,  kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Arumeru ambaye ni Mwenyekiti ya Kamati ya Mashirika hayo, kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Ausha.


Msajili Msaidizi wa NGO's halmashauri ya Arusha, Ahadi Mlai akitoa ufafanuzi wa uwasilishaji wa taarifa za mashirika, wakati wa kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Ausha.


Mwakilishi wa shirika la CWCD akiwasilisha taarifa ya shirika lake, wakati wa kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Ausha.






Mwakilishi wa shirika la Kids Care International - Tanzania, Glory Swai, akiwasilisha taarifa ya shirika lake, wakati wa kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Ausha.




Wawakilishi wa Mashirikia wakifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa kikao cha kuwasilisha taarifa za mashirika yasiyo ya kiserikali, kwenye ukumbi wa mikutano, halmashauri ya Arusha.









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.