• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Nidhamu yatajwa kuwa msingi wa maandalizi ya mashindano ya UMISETA Arusha DC

Posted on: May 3rd, 2018

Wanafunzi na wanamichezo wanaoshiriki michezo ya shule za sekondari 'UMISETA', halmashauri ya Arusha, wametakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika michezo hiyo,  jambo ambalo litawapeleka kwenye mafanikio ya ushindi.

Rai hiyi imetolewa na Mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera,  wakati wa uzinduzi wa Bonanza la UMISETA lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari ya Ilboru mwishoni mwa wiki iliyopita.

Dkt. Mahera amewataka wanafunzi hao kuwa nidhamu wakati wote wa mashindano hayo, kwa kuwa nidhamu ndio msingi mkuu, si kwa michezo tuu hata katika taaluma pia.  

Ameongeza kuwa nidhamu ndio nguzo ya mafanikio kwaa mtu yoyote, na kufafanua kuwa,  watu wengi waliofanikiwa ni wenye nidhamu, kuanzia nyumbani, kwa jamii, shuleni mpaka katika kutekeleza majukumu yao wawapo kazini.

 "Mwanafunzi mwenye nidhamu anayo nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri kitaaluma,  pamoja na kufika mbali kwa kupata mafanikio hata ya kimaisha" amesema Dkt.

Aidha Dkt. Mahera amefafanua kuwa,  michezo ni afya ya kufanya mwili kuwa 'active' na kuifanya akili kuweza kufanya kazi kwa weledi pamoja na kuleta upendo, kufahamiana na kushirikiana.

Hata hivyo mkurugenzi huyo,  amewataka walimu na makocha kuunda timu mahiri zenye wachezaji wanaojituma katika mashindano hayo ili kupata ushindi kuanzia ngazi ya mkoa mpaka taifa.  

Naye Afisa Utamaduni na Michezo, halmashauri ya Arusha, mwalimu Gasper Tesha, amesema kuwa Bonanza hilo linafanyika kwa kushindanisha timu kutoka kanda 5 za halmashauri hiyo kwa lengo la kuchakua na kupata wachezaji bora watakaounda timu zitakazowakilisha halmashauri kimkoa kuanzia tarehe 26.05.2018.

Tesha ametaja michezo itakayoshirikishwa ni pamoja na soka la wavulana na wasichana, mpira wa pete, kikapu, wavu,meza,riadha, bao na michezo ya sanaa na maonesho.

Hata hivyo Tesha ameongeza kuwa, Bonanza hilo limeshirikisha jumla ya wanafunzi 120 wakike na kiume, lakini watachujwa na kubaki wanafunzi 90 ambao wataunda timu za michezo yote na kuwakilisha halmashauri kimkoa.

Rahma Saida mwanafunzi wa shule ya sekondari Oldadai,  na mchezaji kutoka kanda ya Sokoni II, ameahidi kufanya vizuri katika mashindano hayo na amewataka wazazi  kuwaandaa watoto wakike kujitambua ili wawaruhusu kushiriki michezo kwa kuwa wazazi wengi, huwazuia watoto wao wa kike kushiriki michezo kwa kuhofia kujiingiza kwenye vitendo vibaya.

Naye Amir Waziri wa Kanda ya Ilboru amesema kuwa wamejipanga kufanya vizuri kwenye mashindano hayo mpaka ngazi ya taifa licha ya changamoto za ukosefu wa viwanja vya michezo vyenye viwango kwenye shule zao.

Kanda zitakazoshiriki Bonanza hilo ni pamoja na kanda ya Sokoni II,  Ilboru, Kisongo, Mlangarini na Kiranyi ambazo zimtoa wachezaji kutoka shule za sekondari katika maeneo hayo.

Michezo ya UMISETA kitaifa yanatarajiwa kufanyika kitaifa mkoani Mwanza yenye kauli mbiu ya  'Michezo, Sanaa, Taaluma ndiyo Msingi wa Maendeleo'.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.