• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

NMB KUBORESHA USHIRIKIANO NA HALMASHAURI YA ARUSHA

Posted on: August 16th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Benki ya NMB kanda ya Kaskazini, imeahidi kuendelea kuboresha na kudumisha ushirikiano baina yake na halmashauri ya Arusha, katika kutekeleza shughuli mbalimbali za kibenki na za kijamii, lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi.

Makubaliano hayo yamefanyika wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha pamoja mameneja wa matawi ya NMB Arusha na Wakuu wa Idara na vitengo, halmashauri ya Arusha, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Palace Hotel Arusha jijini Arusha.

Mameneja hao, wamepata wasaa wa kuelezea fursa mbalimbali za kibiashara na kijamii zinazotolewa na benki hiyo , wakijipambanua zaidi ya kuweka, kutoa na kukopa fedha, huduma ambazo ni pamoja na ushauri wa kibiashara na uwekezaji kwa wafanyabiashara binafsi, mashirika, kampuni na hata Taasisi za serikali ikiwemo halmashauri.


Meneja wa NMB tawi la Clock Tower, Emmanuel Kishosha, amewataka watalamu hao wa halmashauri, kushirikiana na watalamu wa benki kwa kutumia fursa hizo kulingana na huduma zinazotolewa na mahitaji ya halmashauri lengo likiwa ni kufikia malengo ya serikali ya kuwahudumia watanzania.

"NMB inahudumia watumishi mmoja mmoja, lakini pia inatoa huduma nyingine nyingi kwa taasisi, inatoa huduma kwa vikundi vya wakulima, wafugaji, wajasiriamali pamoja na kutumia  1% ya faida yake kuirudisha kwenye jamii kwa kutoa misaada katika sekta ya Elimu na Afya ambayo inakwenda moja kwa moja kwa wananchi katika halmashauri zenu" Ameweka wazi Kishosha.

Hata hivyo watalam wa halmashauri ya Arusha, licha ya kuushukuru uongozi wa benki hiyo, wamekiri kupata uelewa wa ziada wa huduma zinazotolewa na benki hizo, huduma ambazo hawakuzifahamu hapo awali na kuahidi kushirikiana na benki hiyo kwa kutumia fursa zilizopo.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, ameweka wazi kuridhishwa na huduma zinazotolewa na benki hiyo na kuitaka benki hiyo kukaribia na kuwekeza kwenye halmashauri hiyo, kutokana na kuwa na maeneo ya uwekezaji ambayo yatawezesha kurahisisha huduma kwa wananchi wa halmashauri hiyo.

"Licha ya kwamba mnatoa huduma kupitia asilimia 1 ya faida, lakini tuwaombe kupitia kitengo cha uwekezaji, kuwekeza katika Halmashauri yetu, kwa kuwa kuna maeneo ambayo yanafaa kwa uwekezaji, jambo ambalo litawezesha halmashauri kupata manufa na benki kupata faida

Kikao kazi hicho kimefungua ufahamu kwa watumishi juu ya huduma zinazotolewa na benki hiyo, huku kwa pamoja wakikubaliana kushirikiana hata katika shughuli za kibenka na zile za kijamii.


SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI

JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022












Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.