Na. Elinipa Lupembe.
Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Ufundi Stadi, na utekelezaji wa miradi ya Lipa kutokana na matokeo 'Education Payment for Result' (EP4R), imeweza kuboresha miundombinu ya shule katika halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru kwa miaka mitatu mfululizo sasa.
Mkakati huo wa serikali ya awamu ya tano, wenye lengo la kupandisha kiwango cha taaluma shuleni, kwa kuwezesha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, umeendelea kuleta mafanikio chanya kwa shule za msingi na sekondari nchini.
Shule ya sekondari Mlangarini, ni moja ya shule iliyonufaika na miradi hiyo, mara baada ya shule hiyo, kupata hadhi ya kuwa na wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita 'High School' mwaka 2016, kwa kuletewa fedha za ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule ili kuendana na hadhi ya shule za kidato cha tano na sita.
Kwa mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 250 kwa shule hiyo, na kufanikiwa kujenga vyumba 6 vya madarasa, bweni la kulala wasichana 70 wa kidato cha tano na sita, ukarabati wa maabara za masomo matatu ya Sayansi pamoja na ujenzi wa vyoo vya wanafunzi.
Hata hivyo kutokana matokeo mazuri ya usimamizi wa miradi hiyo, mwaka huu wa fedha 2018/2019, serikali imetoa tena fedha shuleni hapo, kiasi cha shilingi milioni 110, kwa ajili ya ujenzi wa Maktaba na ukarabati wa bwalo la chakula, ujenzi ambao unategemea kukamilika kabla ya kumalizika mwaka huu wa fedha, unaoishia Juni 2019.
Hata hivyo uongozi wa halmashauri ya Arusha, unawataka wananchi na wadau wote wa elimu ndani na nje ya halmashauri, kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Dkt. John Magufuli, kwa kuchangia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya shule za serikali, ili kuhakikisha mtoto wa kitanzania kutoka familia masikini naye anapata elimu katika mazingira bora na rafiki.
*PICHA ZA MAJENGO YA P4R SHULE YA SEKONDARI MLANGARINI*
Jengo la maabara za masomo ya Baiolojia, Kemia na Fizikia shule ya sekondari Mlangarini, imekamilishwa na mradi wa EP4R.
Vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini, yamejengwa na fedha za mradi wa EP4R.
Vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini, yamejengwa na fedha za mradi wa EP4R.
Muonekano wa vyumba sita vya madarasa ya kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini.
Bweni la wanafunzi wa kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini, yamejengwa na fedha za mradi wa EP4R.
Muonekano wa nyuma wa Bweni la wasichana la wanafunzi wasichana wa kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini, yamejengwa na fedha za mradi wa EP4R.
Muonekano wa ndani wa Bweni la wasichana la wanafunzi wasichana wa kidato cha tano na sita shule ya sekondari Mlangarini, yamejengwa na fedha za mradi wa EP4R.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.