Na Elinipa Lupembe
Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela ameagiza waliojenga nyumba ndani ya mita 10 za barabara ya Mianzini , Timbolo, Sambasha hadi Ngaramtoni, kubomoa nyumba zote hizo, kabla ya tarehe 26, Desemba 2022, ili kupisha ujenzi wa barabara unaoendelea.
Mkuu huyo wa mkao ametoa kauli hiyo alipotembela na kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Km 18, inayojengwa kwa kiwango cha lami, mradi unaotekelezwa katika halmashauri za Jiji la Arusha na Arusha, utakaogharimu shilingi bilioni 22 hadi kukamilika kwake na kwa sasa ujenzi umefikia asilimia 8.
Mongella amefafanua kuwa kwa mujibu wa sheria ya barabara ya mwaka 2007 upana wa barabara ulitakiwa kuwa mita 20 kila upande, lakini serikali ya Rais Samia inayowajali wananchi wake na haitaki wapate kero hivyo imepunguza na kuwa mita 10 kwa kila upande.
Aidha amewataka wananchi wa maeneo ambayo barabara hiyo inapita, kutoa ushirikiano ikiwa ni kuunga Mkono juhudi za serikali kwa kuwa barabara hiyo inaleta maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
"Serikali imeshaleta fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii, haiwezekani ikacheleweshwa na watu wachache wasiotaka kubomoa nyumba zao, wananchi changamkieni fursa hiyo, kuna fursa pia ya ajira wakati ujenzi huu unavyoendelea " Amesema mkuu wa mkoa huyo.
Aidha, ameitaka Wakala wa barabara Tanzania (TANROAD) kuendelea kutoa elimu ya sheria ya barabara kwa wananchi ili waweze kuifahamu vizuri na kujenga uelewa wa pamoja.
Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Arusha Muhandisi Regnand Massawe amesema barabara hiyo ya Mianzini Sambasha ina urefu wa KM 12 na ile inayoanzia Olemringaringa hadi Ngaramtoni ina urefu wa KM 6 na kufanya jumla ya Km 18 na ujenzi unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 2023.
Hata hivyo baadhi ya wananchi wameishukuru serikali kwa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami na kuitaka serikali kusimamia sheria kwa usawa ili kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo bila vikwazo.
"Serikali isimamie sheria kwa watu wote, wananchi tunataka maendeleo, hao wachache wanaokwamisha wachukuliwe hatua, ili wapishe ujenzi wa barabara uendelee, tumesubiri lami kwa muda mrefu, wakati umefika sasa". Amesema Zelote Aloyce mkazi wa Mianzini
Ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa ya kukagua ujenzi wa barabara ya Mianzini, Timbolo - Kinyaki hadi Ngaramtoni ilikuwa na lengo la kukagua ujenzi pamoja na kusikiliza changamoto za wananchi wa maeneo hayo.
ARUSHA DC
KaziIendelee✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.