"Nendeni mkabainishe changamoto zilizopo katika jamii nakuzitatua kulingana na mazingira yake".
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella alipokuwa akifungua semina kwa mashirika yawazawa yanayojishughulisha na shughuli za afya Mkoani Arusha na Morogoro.
Ameyataka mashirika hayo yakajenge mahusiano mazuri na Serikali katika maeneo yao ya kazi ili kukuza mchakato mzima wa maendeleo.
Vilevile, ameshauri utaratibu huo wa kuyajengea uwezo mashirika hayo uweze kuwafikia na watendaji wa ngazi za chini zaidi ili kwa pamoja kuwe na uwelewa mmoja kwa wote.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Silvia Mamkwe amewashukuru wadau hao kwa kuendelea kushirikiana na Serikali hususani maswala ya afya.
Amewaomba waendelee kutoa ushirikiano huo ili kuleta maendeleo katika jamii yetu.
Semina ya kuyajengea uwezo mashirika ya wazawa imeandaliwa na shirika la USAID Jijini Arusha kwa lengo la kuyafanya mashirika hayo yaweze kusimama yenyewe katika kutatua changamoto za jamii zao.
SOURECE: OFISI YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
#KaziIendelee
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.