Na Elinipa Lupembe
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella amekagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu shule ya sekondari Kiutu, mradi unaotekelezwa na serikali kwa gharama ya shilingi milioni 98 kupitia mradi wa kuboresha miundombinu ya shule za sekondari (SEQUIP)
Mradi huo ukiwa kwenye hatua ya kupaua, Mkuu huyo wa mkoa ameshauri kuzingatia matumizi ya mbao bora zilizokauka ili kuepuka kupinda hapo baadaye na kuwasisitiza watalamu kuendelea kuzingatia hali ya ubora wa ujenzi unaofuata hatua na taratibu ili mradi ukamilike kwa wakati ukiwa na ubora unaozingatia thamani ya pesa iliyotolewa na serikali.
Ikumbukwe kuwa serikali ilitoa milioni 585kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo ya sekondari Kata ya Kiutu na sasa imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu yenye sehemu ya kuishi familia mbili ( 2 in 1) lengo likiwa kuhakikisha walimu wanaishi karibu na shule ili kuwarahisishia kazi za utekelezaji wa majukumu yao ya kufundisha.
Mkuu huyo wa mkoa, anafanya ziara ya siku mbili 18- 19.09.2023 ya kukagaua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya Elimu sekondari na Msingi, miundombinu ya barabara na maji, pamoja na kufanya mikutano ya hadhara na kusikiliza kero za wananchi katika kata za Oldonyowas na Bwawani.
Arusha DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.