• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERA YA DIPLOMASIA YA UCHUMI YA TANZANIA INAVYOVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI.

Posted on: December 20th, 2023



Na.Arusha DC

Msimamo wa Serikali ya awamu ya sita katika kukuza sera yake ya Diplomasia ya Uchumi, imeendelea kuifungua nchi kwani taasisi ya SALMIN AFRIKA yenye makao makuu yake Dubai kwa kushirikiana na Taasisi ya KGB FUND- VIETNAM zimekuja Mkoani Arusha kwa lengo la kuangalia fursa za uwekezaji zitakazowashirikisha wazawa.

Akizungumza wakati wa kikao hicho cha uwekezaji, Rais wa Taasisi ya SALMIN AFRIKA Profesa Salmin Ibrahim Salmin amesema kuwa, kazi kubwa ya Taasisi yake ni ushauri wa kiuwekezaji pamoja na kuwatafuta wawekezaji wakubwa wenye mitaji pamoja na Taasisi za kifedha zenye riba nafuu ili kuwaunganisha na Watanzania ambao wana makampuni yaliyosajiliwa ili waweze kuingia makubaliano ya uwekezaji.

Profesa, Salmin ameeleza kuwa, Tanzania imebahatika kuwa na fursa nyingi za uwekezaji hivyo kwa kutambua hilo, wameona ni vyema kuwaunganisha Watanzania na fursa za mikopo ya riba nafuu pamoja na wawekezaji wakubwa wenyewe mitaji kwa lengo la kufanya uwekezaji na biashara kwa ushirikiano wa pamoja. “Kampuni ya KGB FUND ya Vietnam ni moja ya kampuni tuliyoileta nchini na iko tayari kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo cha mpunga, ufugaji na uvuvi wa samaki, uanzishaji wa viwanda vya samani zinazotokana na mbao, uchimbaji madini pamoja na ununuzi wake, ujenzi wa mahoteli pamoja na nyumba za makazi, biashara ya utalii pamoja na viwanda vya kusindika matunda na chakula”, ameweka wazi.

Kwa upande wa mikataba ya uwekezaji na biashara, Profesa Salmin amesema Taasisi yake itafuata Sheria na taratibu za nchi katika masuala ya uwekezaji kwa kuhakikisha kampuni za wazawa wanaotaka kuingia nao mikataba ya ushirikiano, zinakuwa na leseni halali za kibiashara pamoja na kutumia taratibu za kibenki katika kuwawezesha wale wote watakaofuzu vigezo vya kupata mikopo ya riba nafuu na yenye marejesho ya muda mrefu.

Akizungumzia fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Arusha hususan katika Halmashauri ya Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, ndugu Seleman Msumi amesema Halmashauri inayo maeneo yanayofaa katika uwekezaji wa mahoteli, nyumba za makazi, viwanja vya michezo, maeneo ya kujenga masoko ya kisasa, ujenzi wa vituo vikubwa vya magari ya abiria na mizigo, maeneo ya ujenzi wa vituo vya afya vya kutolea huduma ya dharura pamoja na kumbi za mikutano ya kimataifa. Maeneo hayo yapo burka A na B, Gomba Estate, Mateves, Ngaramtoni, Likamba pamoja na Mlangarini.

Msumi anasema, maeneo hayo yapo kwenye ukanda maalum kiuwekezaji na kuwa yametengwa mahususi ili kuongeza vitega uchumi vya Halmashauri, ambapo moja ya jukumu kubwa la Halmashauri hiyo ni kubuni vyanzo vipya vya mapato pamoja na kukusanya maduhuri kupitia vyanzo hivyo.

Aidha, ndugu Msumi pamoja na kuipongeza Taasisi hiyo kwa kuonyesha dhamira ya kuwaleta wawekezaji na kutafuta Taasisi za kifedha zenye riba nafuu, pia amewataka kuzingatia taratibu na Sheria za uwekezaji hususan wakati wa utengenezaji wa mikataba, ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima wakati wa utekelezaji wake.

Itakumbukwa kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh.Dkt Samia Suhulu Hassan tangu kuingia kwake madarakani, imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali ikiwemo kufanya mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje, ili kuimarisha uchumi wetu kama nchi hasa baada ya kutoka katika janga la uviko 19.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.