Na Elinipa Lupembe.
Serikali ya awamu ya sita inaomkakati wa kukamilisha ujenzi wa maboma yaliyojengwa na wananchi katika maeneo ya vijiji vya halmashauri ya Arusha baadaya serikali kufanya tathmini na kujiridhisha.
Hayo yamewekwa wazi na mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, seleman Msumi, akijibu swali lililoulizwa na Diwani wa kata ya Oldonyosambu Mhe. Raymond Lairumbe kwenye kipindi cha Maswali ya Papo kwa Papo, kwenye mkuatano wa Baraza la Madiwani la robo ya nne kwa mwaka wa fedha 2022/2023,
aliyetaka kufahamu ni lini serikali itachukua hatua za kukamilisha miradi iliyojengwa kwa nguvu za wananchi na kufikia hatua za boma.
"Tunafahamu serikali ilihamasisha wananchi kuanzisha ujenzi wa miradi mbalimbali kulingana na vipaumbele kwa ahadi ya kufikisha hatua ya boma na baadaye Serikali kumalizia, wanachi walijikusanya na kujitoa kuanzisha ujenzi wa miradi hiyo, lakini mpaka sasa miradi mingi imeishia kwenye maboma, Je ni lini Serikali itakamilisha maboma hayo ili kuwatia moyo wa kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo yao?. Ameulia Mhe. Lairumbe.
Hata hivyo Mkurugenzi Msumi amesema Serikali ilitoa agaizo la kubainisha maboma yote ndani ya halmashauri na kupata jumla ya maboma 54 ambayo tayari yaliwasilishwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, na tayari timu ya watalamu kutoka TAMISEMI walifika na kufanya tathmini ya maboma yote na tayari serikali iko kwenye utaratibu wa kuakamilisha maboma hayo.
"Tayari tulishawasilisha jumla ya maboma 54 ambayo yanahitaji shilingi bilioni 1.8 ili yaweze kukamilisha ujenzi wa maboma hayo, na tayari tunasubiri utekelezaji wa maboma hayo.
Aidha Mkurugenzi Msumi amefafanua kuwa, katika mwaka huu wa fedha 2023/24, halmashauri imetenga shilingi milioni 258 kwa ajili ya kukamilisha maboma manne ambayo yatakamilika mwaka huu wa fedha kadri mapato yatakavyopatikana.
Ameyataja maboma hayo ni pamoja na ukamilishaji wa jengo la utawala Kituo cha Afya Mateves milioni 80, ukamilishaji wa jengo la mama na mtoto kituo cha Afya Oldonyosambu milioni 70, ukamilishaji wa shule mpya ya sekondari Kiutu milioni 90 na Bweni la shule ya sekondari Kimnyaki milioni 18.
Awali mkutano wa baraza la madiwani wa robo ya nne wa kuanzia Aprili - Juni 2023, unafanyika kwa mujibu wa kanuni sheria na taraibu za uendelshaji wa vikao vya halmashauri
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.