• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YA AWAMU YA SITA ILIVYOIPAISHA SEKTA YA AFYA NCHINI

Posted on: April 25th, 2025



SERIKALI YA AWAMU YA SITA ILIVYOIPAISHA SEKTA YA AFYA NCHINI



Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko leo tarehe 25 Aprili,2025 amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha na kujiona jitihada za Serikali ya awamu ya sita katika kuboresha sekta ya afya nchini huku akisisitiza kuwa mafanikio  hayo ni matokeo ya uongozi thabiti chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. 



Dkt. Biteko ameyasema hayo alipotembelea na kukagua mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Meru iliyopo Tengeru Wilayani Arumeru ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake kwa baadhi ya Wilaya Mkoani Arusha.



Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kupongeza thamani ya fedha za umma zilivyotumika kwa ufanisi huku akisisitiza kuwa huduma bora kama hizo ni matokeo ya mipango madhubuti ya Serikali ya awamu ya sita.


“Huduma bora namna hii siyo bahati mbaya, ni matokeo ya uongozi makini na maono ya mbali ya Rais Samia. Hapa tumeona ubora ukizingatiwa sambamba na thamani ya fedha zilizotumika”. Amesema.



Sambamba na hilo,Dk.Biteko amesisitiza umuhimu wa kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo ili iweze kuwanufaisha jamii kwa muda mrefu na pia akatoa wito kwa wananchi kudumisha mshikamano wa Kitaifa kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisi na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Aman Karume Rais wa Kwanza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, amesema kuwa Mkoa Arusha umeandaa mkakati wa kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kuanzisha ushirikiano wa kimatibabu na utaalam toka kwa madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuwapunguzia wananchi gharama kubwa za matibabu.


“Tunalenga kuwa na hospitali moja maalum ya rufaa itakayoshirikiana na madaktari bingwa kutoka nje ya nchi na ndani ili kutoa huduma bora kwa wananchi wetu hasa wale wa kipato cha chini waweze kunufaika na huduma hiyo ya matibabu.” Amesema Mhe. Makonda.


Mradi huo umetekelezwa kwa 'force account' kwa gharama ya shilingi milioni 900 zilizotolewa na Serikali Kuu, na hadi sasa umekamilika kwa asilimia 100, hivyo kuongeza uwezo wa hospitali kutoa huduma bora kwa wananchi.




Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko leo tarehe 25 Aprili,2025 amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha na kujiona jitihada za Serikali ya awamu ya sita katika kuboresha sekta ya afya nchini huku akisisitiza kuwa mafanikio  hayo ni matokeo ya uongozi thabiti chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. 



Dkt. Biteko ameyasema hayo alipotembelea na kukagua mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Meru iliyopo Tengeru Wilayani Arumeru ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake kwa baadhi ya Wilaya Mkoani Arusha.



Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kupongeza thamani ya fedha za umma zilivyotumika kwa ufanisi huku akisisitiza kuwa huduma bora kama hizo ni matokeo ya mipango madhubuti ya Serikali ya awamu ya sita.



“Huduma bora namna hii siyo bahati mbaya, ni matokeo ya uongozi makini na maono ya mbali ya Rais Samia. Hapa tumeona ubora ukizingatiwa sambamba na thamani ya fedha zilizotumika”. Amesema.



Sambamba na hilo,Dk.Biteko amesisitiza umuhimu wa kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo ili iweze kuwanufaisha jamii kwa muda mrefu na pia akatoa wito kwa wananchi kudumisha mshikamano wa Kitaifa kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisi na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Aman Karume Rais wa Kwanza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, amesema kuwa Mkoa Arusha umeandaa mkakati wa kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa kuanzisha ushirikiano wa kimatibabu na utaalam toka kwa madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuwapunguzia wananchi gharama kubwa za matibabu.



“Tunalenga kuwa na hospitali moja maalum ya rufaa itakayoshirikiana na madaktari bingwa kutoka nje ya nchi na ndani ili kutoa huduma bora kwa wananchi wetu hasa wale wa kipato cha chini waweze kunufaika na huduma hiyo ya matibabu.” Amesema Mhe. Makonda.



Mradi huo umetekelezwa kwa 'force account' kwa gharama ya shilingi milioni 900 zilizotolewa na Serikali Kuu, na hadi sasa umekamilika kwa asilimia 100, hivyo kuongeza uwezo wa hospitali kutoa huduma bora kwa wananchi.


Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.