• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAAHIDI KUONGEZA FEDHA KUMALIZIA UKARABATI MIUNDOMBINU SEKONDARI ILBORU

Posted on: August 19th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

      Serikali imeahidi kutafuta fedha nyingine, kwa ajili ya kukamilisha ukarabati wa miundombinu ya shule ya sekondari Ilboru, ikiwemo baadhi ya vyumba vya madarasa, mabweni, vyoo na mabafu pamoja na nyumba za walimu, miundombinu iliyojengwa kabla ya kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika.

       Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, Mheshimiwa Mwita Waitara, alipotembelea shuleni hapo, kukagua utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa shule hiyo ya sekondari Ilboru, uliofanywa na serikali kupitia fedha zilizotolewa na Mamlaka ya Elimu Tanzania - TEA za ukarabati wa shule kongwe nchini.

      Naibu Waziri huyo ametoa ahadi hiyo, baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa awamu ya kwanza,mmradu ambao licha ya kukamilika kwa fedha zilizotolewa lakini bado shule hiyo kongwe, inahitaji ukarabati kwenye miundombinu ambayo haikufikiwa wakati wa awamu ya kwanza ya ukatabati wa shule hiyo, ikiwemo mabweni, baadhi ya vyumba vya madarasa na nyumba za walimu, mradi unaotegemea kugharimu shilingi milioni 900.

   "Kwa hali niliyoiona ya majengo ya zamani, na taarifa mliyonipa, kunauhitaji wa ukarabati wa miundombinu iliyobaki, tunakwenda kuangalia namna ya kuingiza shule ya Ilboru kuweza kupata fedha, milioni 900 za kumalizia ukarabati huo, ni kweli majengo yamechoka kutokana na kujengwa miaka mingi iliyopita". amefafanua Naibu Waziri huyo.

   Hata hivyo Naibu Waziri, amewasihi viongozi wote kuanzia ngazi ya wilaya, halmashauri na shule pindi watakapopata fedha hizo, kutumia forced account na mafundi wazawa 'local fundi', pamoja na kuzisimamia fedha hizo kwa karibu na umakini ziweze kukamilisha ukarabati huo, kwenye maeneo yaliyobaki.

        Ameweka wazi kuwa, licha ya kukamilika awamu ya kwanza ya ukarabati iliofanyika kweye shule 86 nchini, Serikali imejipanga kuanza kufanya ukarabati wa shule za kawaida na zile za kata, mara baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya ukarabati wa shule zake kongwe, ikiwmo shule ya sekondari Ilboru.

      Naye Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, amemuahidi Naibu Waziri huyo, kusizimamia fedha hizo na kukahikisha zinatumika kulingana na maelekezo ya serikali, mara tuu serikali itatekeleza ombi lao, la kumalizia ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo iliyobaki, ikiwemo nyumba za walimu.

        "Mheshimiwa Naibu Waziri, tunakushukuru na tunakupongeza wewe na serikali, serikali makini nayoongozwa na Jemadari, Rais wetu Dkt. John Magufuli, kwa kuijali wilaya ya Arumeru, wilaya hii ni moja ya wilaya inayopendelewa kwa kupata fedha nyingi za miradi hasa katika sekta hii ya elimu na afya, nikuahidi kuendelea kusimamia matumizi sahihi ya fedha yoyote ya serikali, itakayoletwa katika wilaya yangu". amesisitiz mkuu huyo wa Wilaya.

    Naye mkuu wa Shule ya sekondari Ilboru, amesema kuwa shule ya sekondari Ilboru, ni shule moja ya shule kongwe nchini inayofanya vizuri kitaaluma, ilianza rasmi mwaka 1946 kabla ya Uhuru wa Tanganyika, ikiwa sasa na  jumla ya wanafunzi 817 wavulana, na ina jumla ya vyumba vya madarasa 18.


PICHA ZA MATUKIO ZIARA YA NAIBU WAZIRI ILBORU SEKONDARI






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.