• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YABORESHA MIUNDO MBINU ZAHANATI MWANDETI KUWA KITUO CHA AFYA

Posted on: February 7th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Serikali ya awamu ya sita imeendelea kuboresha  huduma za afya nchini, huku halmashauri ya Arusha ikiwa ni miongoni mwake, kwa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi hasa maeneo ya vijijini, lengo likiwa ni kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo za afya sambamba na  kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Katika kutimiza adhma hiyo, serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 490 kwa ajili ya upanuzi wa zahanati ya Mwandeti,  ili kuipa hadhi ya kuwa Kituo cha afya, kiweze kutoa huduma nyingi  zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo awali ikiwa ni zahanati.

Akizungumza na mwandishi wetu, mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amebainisha kuwa, halmashauri imepokea kiasi hicho cha fedha, kwa awamu tatu tofauti, kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu katika  zahanati ya Mwandeti ili kikipandisha hadhi na kuwa Kituo cha Afya.

Ametaja mchanganuo wa shilingi milioni 490, kimetumika kujenga miundo mbinu ya majengo,  ikiwa ni pamoja na jengo la mama na mtoto 'maternity ward' na jengo la upasuaji 'theater', kwa shilingi milioni 150, milioni 259 zinajenga jengo la Wagonjwa wa nje ' OPD', Maabara na kichomea taka, huku milioni 90 zikitumika kujenga nyumba moja ya watumishi yenye uwezo wa kuishi familia tatu (3 in 1).

"Nipongeze serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mama Samia Suluhu Hassan, kwa kuwakumbuka na kuwahurumia kina mama wajawazito na watoto, waliokuwa wanahatarisha maisha na wengine kupoteza maisha wakati wa kujifungua, kutokana na kukosa huduma za haraka wakati wa kujifungua, uwepo wa Kituo cha afya Mwandeti kutapunguza ama kuondoa kabisa vifo visivyo vya lazima" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Aidha Msumi ametaja mchanganguo wa fedha hizo, shilingi milioni 490, kulingana na vyanzo vyake kuwa shilingi milioni 240 kutoka serikali Kuu, lakini shilingi milioni 250 fedha kutoka serikali Kuu, kupitia tozo ya miamala ya simu, tozo ambazo watumiaji wote wa simu nchini wanachangia maendeleo ya nchi yao, ikiwemo wananchi wakazi wa Mwandeti. 

Naye Mganga Mfawidhi, Zahanati ya Mwandeti, Dkt. Aidan Martin, amesema kuwa, uwepo wa kituo cha afya Mwandeti, utasaidia upatikanaji wa huduma muhimu ambazo hapo awali, zilikuwa hazipatikani kwenye zahanati, huku wagonjwa wakilazimika kwenda hosptiali ya wilaya ya Olturumeti umbali wa zaidi ya Kilomita 35, jambo lililoongeza gharama na kuhatarisha maisha ya wagonjwa.

"Tulikuwa tunatoa rufaa nyingi kwa wagonjwa, lakini uwepo wa kituo cha afya, tunatarajia huduma nyingi zitapatikana hapa na kutakuwa na oingezeko la wagonjwa kutoka wastani wa wagonjwa 1,200 mpaka 1,700 kwa mwezi" ameweka wazi Daktari Aidan.

Hata hivyo wananchi wa kata ya Mwandeti husasani kijiji cha Engalaoni, ambao hutumia zahanati Mwandeti kwa matibabu, wameishukuru serikali kwa kuona umuhimu na kuwapa fedha za kuongeza miundo mbinu ya majengo, ili zahanati hiyo ipandishwe hadhi na kuwa kituo cha afya jambo ambalo wamethibitisha kuwa Mungu amewaonekania kwa kusikia kilio chao.

Diwani wa kata ya Mwandeti, Mhe. Logolie Lukumay amethibitisha kuwepo kwa changamoto zakupata matibabu kwa wagonjwa wa kijiji cha Engalaoni, hasa kwa kuzingatia kijiji hicho ni cha mwisho wa kata na wilaya pia.

Amesema kuwa, kiwepo kwa Kituo cha afya, licha ya wananchi kuwa na uhakika wa kupata matibabu kituoni hapo, lakini pia kitapunguza gharama za kusafiri umbali mrefu kupata matibabu kwenye hospitali kubwa na zaidi, kitasaidia kupunguza vifo visivyo vya lazima hasa kwa kina mama wajawazito wanaohitaji kufanyiwa upasuaji pamoja  na watoto  wanazozaliwa.

."Tunaishukuru serikali ya awamu ya sita, tunamshukuru sana mama Samia Suluhu, ametufuta machozi ya muda mrefu, zahanati hii inahudumia watu wa Engalaoni na kata jirani ya Monduli, lakini watu waliteseka sana kupata matibabu, kina mama wajawazito wanapohitajika kufanyiwa 'operation' ilikiwa ni shida sana, usafiri nao ilikuwa  shida na umbali pia wa kufika hospitali ya wilaya ilikuwa ni tatizo" amefafanua Mheshimiwa Logolie.

Kukamilika kwa ujenzi wa miundo mbinu ya zahanati ya Mwandeti, kunategemea kukipandisha hadhi na kuwa kituo cha afya, kituo ambacho kitahudumiza zaidi ya watu elfu 15 wa kata ya Mwandeti na kata ya jirani ya Mferejini, wilaya ya Monduli.

ARUSHA DC

#KaziInaendelea✍✍

PICHA ZA MAJENGO MAPYA ZAHANATI YA MWANDETI






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.