Na Elinipa Lupembe
Jumla ya wanafunzi 156 wavulana 77 na wasichana 89 wamepangiwa kuanza kitado cha kwanza shule ya sekondari Likamba muhula wa masomo unaonza Januri 9, 2023 na kuifanya shule hiyo kuwa na jumla ya wanafunzi 358.
Mkuu wa shule ya Sekondari Likamba, Mwl. Richard Mugyabuso amethibitisha kuwa, idadi hiyo ya wanafunzi inakwenda sambamba na uwepo wa vyumba vya madarasa kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha tatu shuleni hapo.
Amesema kuwa shule hiyo ni miongoni mwa shule ambayo inakua kwa kasi kutokana na ukweli kwamba, serikali inaendelea kuongeza nguvu kwa kuimarisha miundo mbinu yake ili iweze kukidhi mahitaji ya wanafunzi kwa ujumla wake.
Mwaka 2019 wananchi wa kijiji cha Likamba waliamua kuunganisha nguvu na kuanza mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya shule ya Sekondari Likamba, kutokana na Jiografia ya kata ya Musa, ilionekana bado watoto wa kijiji cha Likamba walitembea umbali mrefu kufika shule ya kata ya sekondari ya Musa.
Wananchi hao walikusanya pesa na kufanikiwa kujenga vyumba 4 vya madarasa, matundu 8 ya vyoo pamoja na nyumba moja yenye uwezo wa kuishi walimu 8 japokuwa bado hazijakamilika.
Baada ya serikali kuziona juhudi hizo za wananchi hao, ilianza kuweka nguvu kwa kusajili shule hiyo kwa namba S.5349 na hatimaye Januari mwaka 2020, shule ilianza kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza.
Mwaka wa fedha 2020/2021 na 2021/2022 serikali kupitia mradi wa EP4R ilijenga madarasa 4 na baadaye kujenga darasa 1 kwa fedha za mapambano dhidi ya UVIKO 19.
Hata hivyo wananchi wa Likamba walianzisha mradi wa ujenzi wa maabara na baadaye serikaki kukamilisha maabara ya masomo ya Sayansi.
Licha ya mafanikio hayo yote, mwishoni mwa mwaka 2022 serikali pia imetoa shilingi milioni 60 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa, viti na meza 50 kwa kila darasa ikiwani maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza Januari 2023.
Ikumbukwe kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa ni utelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi Ibara ya 79 kifungu (q) Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika shule za Msingi na Sekondari nchini.
ARUSHA DC
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.