• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YATOA VITABU VYA KIADA SHULE ZOTE ZA SEKONDARI ARUSHA DC...

Posted on: September 27th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imetoa jumla ya vitabu vya kiada kwa shule zote za sekondari halmashauri ya Arusha lengo likiwa kuendelea kuboresha miundombinu ya ufundishaji na ujifunzaji kwa walimu na wanafunzi shuleni.


Akizungumza wakati akikabidhi vitabu hivyo kwa wakuu wa shule za sekondari, mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi amesema kuwa halmashauri imepokea jumla ya vitabu vya kiada 26,186 kwa ajili ya shule zote 35 za serikali huku shule tatu mpya za kata zikipokea vitabu 2,720 vya kwa mara ya kwanza na kufanya kwa uwiano wa 1:1 kila mwanafunzi kutumia kitabu chake.


Mkurugenzi Msumi licha ya kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwekeza fedha nyingi za kuboresha miundombinu ya shule za sekondari, amesema kuwa, uwepo wa vitabu shuleni utarahisisha tendo la kufundisha na kujifunza na kuwawezesha wa wanafunzi kujisomea na kupata maarifa zaidi hatimaye kufikia malengo yao ya kitaaluma.


Aidha ametoa wito kwa walimu na wanafunzi kuvithamini vitabu hivyo kwa kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa pamoja na kuvitunza ili viweze kutumiwa sasa  sasa na vizazi vijavyo.


"Niwatake walimu kusimamia utunzaji  na matumizi sahihi ya vitabu hivi na sio kuvifungia stoo, hakikisheni wanafunzi wanavitumia wakati wote wa masomo, huku kukiwa na utaratibu mzuri wa kuviazima na kuvirudisha mara baada ya kuvitumia" Ameagiza Msumi


Hata hivyo wakuu wa shule  wameishukuru serikali kwa kuendelea kuimarisha sekta ya elimu kwa kuhakikisha kuna kuwa na majengo mazuri, vifaa vya kujifunzia pamoja na vitabu vya kiada kwa masomo yote tofauti na miaka ya nyuma changamoto zilikuwa ni nyingi lakini zinaendelea kumalizika siku hadi siku.


Mkuu wa shule ya sekondari Kiutu, Mwl. Upendo Mollel, amesema licha ya kuwa shule yao ni mpya lakini kwa kipindi kifupi serikali imewapa vitabu 1,158 ambapo kila mwanafunzi atatumia kitabu chake mwenyewe jambo ambalo litawaongezea ari ya kujifunza.


"Kabla ya kuwa na vitabu wanafunzi walisoma kwa shida, kitabu 1 wanafunzi 10, wakati mwingine walishindwa kufanya vizuri masomo yao kwa kukosa vitabu vya kufanyia 'reference' uwepo wa vitabu utawapa fursa wanafunzi kujisomea kwa nafasi na kupata maarifa hata baada ya kufundishwa na walimu darasani" Mwl. Jackson Mpinga, Mkuu wa shule sekondari Olomitu


Naye mkuu wa shule sekondari Olturoto, Mwl. Peter Mlinga, amekiri kuwepo tatizo la upotevu wa vitabu shuleni kutokana na uzembe na kuahidi kuandaa mpango mzuri wa utunzaji wa vitabu kwa kumkabidhi kitabu mwanafunzi kwa maandishi na kuhakikisha anatumia na kukirudisha kwa wakati.


Naye Afisa Elimu Taaluma Mwl. Editha Chona, amefafanua kuwa katika mgao huo, wa vitabu 26, 186, shule tatu za mpya za sekondari za kata  zilizosajiliwa kati ya mwaka 2020 na 2023 zimepata vitabu 2,720 vya masomo yote, ikiwa ni pamoja ma  shule  shule ya sekondari Olturoto vitabu 873, sekondari Kiutu vitabu 1,158 na shule ya sekondari Olomitu vitabu 689.


Ikumbukwe kuwa huu ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala ya kuhakikisha mazingira bora ya shule za serikali nchini zikiwa na miundombinu bora, ikiwemo madarasa,  maabara za masomo ya Sayansi na TEHAMA na vifaa vyake, maktaba pamoja na vitabu vya kiada na ziada..


ARUSHA DC NI YETU, TUHSIRIKIANE KUIJENGA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.