• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WANAFUNZI 7, 857  KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 ARUSHA DC..

Posted on: December 22nd, 2022

Na Elinipa Lupembe

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluh Hassan imewahakikishia wanafunzi 7,856 walifaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2022 sawa na asilimia  100, wamepangiwa shule za sekondari za serikali halmashauri ya Arusha

Uthibitisho huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango wakati wa hafla ya makabidhiano ya mradi wa ujenzi wa vymba 38 vya madarasa, vilivyojengwa maalum kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza Januari 2023.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa, kutokana na uwepo wa vyumba vya madarasa 134, ambavyo serikali imewekeza kwa miaka miwili mfululizo vitawezesha idadi hiyo ya wanafunzi kuanza masomo yao mapema Januari 9.

"Mwishoni mwa mwaka 2021 tulipokea shilingi bilioni 2 na kujenga vyumba 96 vya madarasa na mwaka huu tumepokea milioni 769 na kujenga vyumba 38 kwenye shule 18 zilizokuwa na upungufu, madarasa hayo yatatumika kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023". Ameweka wazi Mhandisi Ruyango.

Hata hivyo amewataka viongozi wote kusimamia na kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga na elimu hiyo ya sekondari, wanaanza masomo ifikapo tarehe 9 Januri 2023 na kuwaasa wazazi kuwapatia mahitaji yao ya msingi ya shule kama ilivyo kwenye fomu za kujiunga na shule hizo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojungu Salekwa amethibitisha kuwa, serikali imeshafanya kazi yake, kazi iliyobaki ni kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza wanakwenda shule kwa wakati na kwa idadi kamili ya wanafunzi waliochaguliwa.

"Mama Samia ameshafanya kazi yake, kazi yetu ni moja kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza wanaanza shule kwa wakati, na wazazi kuhakikisha wanawapa watoto wao mahitaji yote ya shule". Amesema Mhe. Ojung'u

Joshua Augustino mwanafunzi anayeingia Kidato cha pili shule ya sekondari Mringa licha ya kuishukuru Serikali kwa kuwajengea nmadarasa mazuri, ameahidi kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yake na kuja kulitumikia Taifa lake la Tanzania.

Mwenyekiti wa Bodi ya shule ya sekondari Mringa Mwl. Jackson Mollel amesema kazi iliyofanywa na serikali ni kubwa na inathamani kwa watoto na vizazi vyao, kazi ambayo imewapunguzia wananchi mzigo wa kuchangia ujenzi wa madarasa, michango ambayo ilikiwa inasuasua na kushindwa hata kukamilisha darasa moja kwa wakati.

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji halmasahuri ya Arusha, Seleman Msumi,  amesema kuwa halmashauri ilipokea shilingi milioni 760 na kujenga vyumba 38 vya madarasa, viti na meza 50 kwa kila darasa pamoja na ofisi 7 za walimu kwenye shule 6 kati ya shule, kwenye shule 18 za sekondari.

Ifahamike kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa ni utelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi Ibara ya 79 kifungu (q) Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika shule za Msingi na Sekondari nchini.



ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.