• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA BUILDERS OF FUTURE AFRICA  LATAMBULISHA MRADI WA KUREJESHA NDOTO ZA KINA MAMA WADOGO...

Posted on: December 24th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Shirika la Builders of Future Africa linalofanya kazi mkoani Arusha limetambulisha mradi wa kuwahudumia kinamama wadogo 'early mothers' kwenye kata tatu za halmashauri ya Arusha, mradi unaotarajiwa kurejesha ndoto zilizotoweka za kina mama hao.

 utakaogharimu shilingi milioni 34.5.

Akizungumza wakati wa kikao cha kutambulisha mradi huo, kilichofanyiaka kwenye ukumbi wa mikutano halmasahuri ya Arusha,  Mkuu wa Idara ya Utumishi na Rasilimali watu, halmashauri hiyo, Elizabeth Ngobei kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, amesema kuwa mradi huu unakwenda kurejesha ndoto na matumaini ya wasichana waliopata mimba za utotoni na kurudi kwenye maisha ya kawaida.

Ameongeza kuwa, mradi huu ni muhimu kwa vijana ambao, waliingia kwenye kadhia ambayo hawakutarajia, na jamii imeonekana kushindwa kukubaliana na uhalisia, jambo ambalo limesababisha wengi kukata tamaa na wengine hata kuchukua maamuzi magumu ya kujiua.

"Ninaamini mnakwenda kufanya kazi ambayo, matokeo yake yatakuwa na manufaa kwa wasichana na watoto wao, kwa familia, kwa jamii na Taifa kwa ujumla, tekelezeni mradi kama ulivyokusudiwa na hakikisheni mnatoa taarifa kwa kila tobo ya mwaka kama taratibu za serikali zinavyoelekeza". Amefafanua Elizabeth

Akitambulisha mradi huo, Mkurugenzi wa shirika la BFA, Elisante Ephrahim amesema kuwa  kwa awamu ya kwanza mradi huo utagharimu shilingi milioni 34.5 na utajihusisha na kutoa elimu ya ujasiriamali kwa kina  mama hao, pamoja na kuwafanya kujitambua na kujithamini.

Amefafanua kuwa shirika limefikia kutekeleza mradi huo, kutokana na changamoto iliyokuwa ikiwakabili wasichana waliopata mimba za utotoni na kujikuta yakipoteza mwelekeo wa maisha kutokana na  kutengwa na familia na jamii, huku ndoto zao kiwa zimeyeyuka.

"Mradi huu unakwenda kurejesha ndoto za kina mama wadogo, kwa kuwajengea uwezo na kuwapa ujuzi na maarifa ya kurejesha matumaini yaliyopotea, ndani ya jamii zetu wasichana waliopata mimba za utotoni, hupitia ukatili na kutegwa na jamii zao, hali inayosababisha kukataa kwa kukatisha ndoto pasi kutegemea". Amefafanua Ephrahim

Mafunzo hayo yatawaunganisha kina mama hao kwenye vikundi vya kuweka na kukopa ili waweze kuanzisha biashara zao kulingana na matakwa yao ili waweze kujikwamu akiuchumi lakini kukabiliana na hali ya ukatili waliupata katika kipindi cha mimba za utotoni.

Hata hivyo madiwani wa kata hizo, wamekiri kuwepo kwa changamoto hiyo katika maeneo yao, huku wakilipongeza na kulishukuru shirika hilo kwa mradi huo, wakiamini ukifanyika kwa kuzingatia vigezo vilivyoainishwa utakwenda kuzaa matunda kwenye jamii zao.

Diwani wa kata ya Mwandeti Mhe. Logolie Lukumay amekirinkuwepo kwa changamoto ya ndoa za utotoni katani mwake hususani kijiji cha Engalaoni na kuongeza kuwa anatamani mrafi huo utekelezwa kwa ukubwa zaidi ili kuwanusuru kina mama hao wadogo pamoja na wachana wanaoendelea kukua.

Naye Msajili wa Mashirika yasiyo ya kiserikali, halmashauri ya Arusha, Ahadi Mlay amelipongeza shirika hilo kwa kufuata taratibu zinatakiwa na serikali na kuyataka mashirika mengine kuiga mfano huo kwa kuwa kazi zote zinatekelezwa kwa kuzingatia vipaumbele vya serikali hususani kwenye uwazi katika utekelzaji wa miradi.

"Niwatake mashirika yote kuzingatia taratibu zote kushindwa kufanya hivyo, shirika litakosa sifa na kufutiwa usajili jambo ambalo halipaswi kutokea, kwa kuwa serikali inawategemea mashirika kuwahudumi wanachi, hakikisheni miradi yote  na gharama zake zinafahamika maeneo husika kwa uwazi" Amesisitiza Ahadi

Awali mradi huo wa nguvu ya binti rika na mama wadogo unategemea kuwafikia wamama wenye watoto  350, na kufanyika kwa miezi 6 kwenye kata za mwandet, Lemanyata Lengijave.


ARUSHA DC



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.