• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA CASEE LAKABIDHI VISHIKWAMBI 55 SHULE YA ENABOISHU ACADEMY - ARUSHA DC

Posted on: April 29th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika lisilo la kiserikali la  Community Aid and Social Education Empowerment -CASEE, kwa ufadhili wa  shirika la Child Fund Korea -CFK la nchini Korea, limekabidhi msaada wa vishikwambi 55, (tablet), kwa shule ya mchepuo wa kiingereza ya Enaboishu Academy, shule inayomilikiwa na halmshauri ya Arusha, lengo likiwa ni kuunga mkono juhudi za za serikali la  kurahisisha na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa walimu na wanafunzi nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Meneja Miradi, shirika la CASEE, Ombeni Sakafu amesema kuwa, wametoa msaada huo wa vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia kwa shule ya msingi Enaboishu Academy, vyenye thamani ya shilingi milioni 30.7, mara  baada ya kupata taarifa, toka kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha, ya  kuwataka wadau kujitokeza kuchangia, maendeleo ya shule hiyo mpya ya mchepuo wa kiingereza, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza na kupandisha taaluma katika shule hiyo na halmashauri kwa ujumla wake.

Sakafu amefafanua kuwa, shirika la CASEE, linafanya kazi kwa kushiriki mipango na malengo ya serikali iliyopo madarakani, kuboresha na kuweka mazingira rahisi na salama ya wanafunzi kujifunzia, hasa kwa kutumia teknolojia ya kisasa, ili kufikia lengo la serikali la kuhakikisha mtoto wa kitanzania anapata elimu bora katika mazingira bora.

"Licha ya kurahisisha tendo la kujifunza na kufundisha kwa kutumia teknolojia ya kisasa, lakini pia CASEE ina lengo pia kuhamasisha wanafunzi kupata masomo kwa njia ya mtandao 'e-learning' na TEHAMA kwa ujumla, tukiamini kujifunza kwa njia ya dijitali, vifaa hivi vitasaidia wanafunzi kupata ujuzi na maarifa, wakati mwingine bila kuwa na mwalimu" amesisitiza Sakafu

Naye Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Arusha na Afisa Elimu Msingi, Hossein Mghewa, amelishukuru shirika hilo la CASEE, kwa kutoa vifaa hivyo vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia, vifaa ambavyo vitarahisisha kazi ya kujifunza na kufindisha kwa walimu na wanafunzi, kwa kuwa vishikwambi hivyo vina programu yenye vitabu vya kiada na ziada, jambo ambalo litapunguza changamoto ya upungufu wa vitabu katika shule hiyo.

"Vishikwambi hivi, vina programu yenye vitabu vya kiada vyenye masomo yote, pamoja na vitabu vya ziada ambavyo vitawaongezea wanafunzi maarifa zaidi kwa urahisi zaidi na gharama nafuu, katika masomo". Amefafanua Kaimu Mkurugenzi huyo.

Hata hivyo Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Msingi Enaboishu Academy, Rajabu Mfutakamba, amesema kuwa, vifaa hivyo ni muhimu sana kwa wanafunzi katika tendo la kujifunza kwa kutumia teknolojia rahisi na ya kisasa, teknolojia ambayo itawezesha kuwajengea maarifa  kupandisha kiwango cha taaluma shuleni hapo.

Mkuu huyo wa shule ameweka wazi kuwa, vishikwambi hivyo vina programu zenye vitabu vya kiada vya masomo yote, vitabu vya ziada kwajili ya kuongeza maarifa katika masomo yao, pamoja na programu maalumu kwa wanafunzi wa awali wanaoanza kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu, maarufu kama  KK tatu.

"Tablet hizi zitasaidia kuwaongezea wanafunzi ari na kasi ya kujifunza pamoja na uwezo wa kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu kwa haraka na wepesi, kutokana na programu yenye kumpa mwanafunzi uwezo wa kusoma na kuandika maneno 200 kwa muda wa dakika 40" amefafanua Mwalimu Mfutakamba

Shirika la CASEE limetoa Vishikwambi 55, kwa shirika la CFK la nchini Korea kufadhili vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milion 30.7, huku fedha hizo zikijumuisha gharama za  vishikwambi 55, vikiwa na kifurushi muhimu 'full package',  pamoja na kiasi cha fedha hizo, kugharamia mafunzo na miongozo ya namna ya kutumia vishkwambi hivyo, kwa walimu wa shule hiyo, ambayo yanaendelea kufanyika.


PICHA ZA MAKABIDHIANO YA VIFAA HIVYO









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.