• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA CCBRT YATOA VITI MWENDO 17 KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WA VIUNGO ARUSHA DC...

Posted on: July 13th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Shirika la CCBRT kanda ya Moshi wametoa viti mwendo 17 kwa watoto 17 wa shule ya msingi na awali,wenye ulemavu wa viungo halmashauri ya Arusha.


Akizungumza wakati wa kukabidhi viti mwendo hivyo, Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mhe. Dkt. Ojung'u Salekwa, amewashukuru wadau wa shirika la CCBRT  kwa msaada huo muhimu na wathamani kwa watoto wenye ulemavu.


Ameongeza kuwa licha ya watoto hao wana na changamoto lakini wazazi wenye watoto wenye ulemavu wanapitia changamoto nyingi zaidi katika malezi hivyo jamii inatakiwa kuungana kutoa msaada wa hali na mali pamoja na kuwatia moyo familia zenye watoto hao.


"Tunalo jukumu kubwa la kuwahudumia watoto wenye ulemavu, kila mtu anayo nafasi kubwa ya kufanya jambo kwa familia hizi kwa kuwa changamoto ya malezi ya watoto hawa ni zaidi ya maisha ya kawaida ya binadamu, tutumie muda hata kuwatia moyo" Amesema Mhe. Mwenyekiti huyo.


Aidha ameipongeza serikali kwa kuweka mazingira bora kwa wadau wa maendeleo na kuwa serikali inathamini kazi kubwa inayofanya na wadau na kuwataka kuendelea kuisaidia serikali katika kuhudumia jamii hususani watoto wenye mahitaji maalum


Naye Mratibu wa Huduma za Viti mwendo  CCBRT Moshi, Neophita Lukiringa amesema kuwa, lengo la shirika kutoa msaada huo ni kwasaidia watoto kuweza kwenda shuleni na kufikia ndoto zao za kielimu lakini pia kuwasaidia wazazi kurahisisha kazi ya kuwahudumia watoto hao.


Hata hivyo wazazi na watoto waliopewa viti hivyo wameshukuru kwa msaada huo, ambao wamekiri ni huduma ambayo walemavu wengi wanaihitaji kwa ajili ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine.


Fatuma Yusuph mama Sahil mtoto wa miaka 9, licha ya kushukuru ameitaka jamii kuendelea kuwasaidi wazazi wenye watoto wenye mahitaji maalum kwa kuwa malezi ya watoto hayo yana gharama kubwa na zaidi yanahitaji mzazi kutumia muda wote bila kufanya shughuli nyingine za uzalishaji.


"Mtoto wangu ana miaka 9 sasa, nahitajika muda wote kuwa nae karibu, ili kumuhudumi, kiwa na kiti mwendo kutanipunguzia kidogo kazi na mimi kupata muda wa kufanya majukumu mengine". Amesema Fatuma


Naye Rachel Mollel mtoto aliyepewa kiti ameishukuru serikali kwa msaada huo, na kuweka wazi kuwa kiti hicho kitamsadia kutembea akiwa shuleni na nyumbani pia.


Hata hivyo mkurugenzi  Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Selema Msumi, licha ya kushukuru kwa msaada huo, amesema kuwa  halmashauri ina watoto 509 wenye uhitaji ambao wanasoma kwenye shule zenye vitengo maalum huku watoto 77 wakisoma kwenye shule ya bweni Ilboru hivyo mahitaji ya watoto hao ni mengi kulingana na idadi yao.


Awali uongozi wa licha ya kuwashukuru wadau, unawataka wadau kuendelea  kujitokeza kuchangia maendeleo ya jamii katika  halmashauri hiyo.


ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA
#kaziiendelee

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.