• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Shirika la EMAC kutoa elimu ya Afya Arusha DC kupitia mradi wa TULONGE AFYA

Posted on: April 18th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Viongozi wa jamii, halmashauri ya Arusha, wamesema kuwa kuna haja ya kutoa elimu kwa jamii yao, juu ya masuala ya afya zao, ili kuweza kujikinga na maambukizi ya magonjwa pamoja na kuzuia madhara makubwa zaidi yanayoweza kutokea kwa jamii kutokana na ukosefu wa elimu ya afya.

Viongozi hao, wamesema hayo wakati wa kikao kazi cha utambulisho mradi wa TULONGE AFYA unaojihusha na masuala ya afya,  unaotekelezwa na shirika lisilo la kiserikali la  'Empowerment of Marginalized Community' - EMAC, kwa ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya nchini Marekani, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SOS eneo la Ngaramtoni.

Akizungumza mara baada ya kuelezwa lengo la mradi, Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Noah Lembris amesema kuwa, kuna haja kubwa kwa jamii kupata elimu zaidi juu ya afya zao, jambo ambalo litawawezesha wananchi kutambua namna ya kujikinga na magonjwa pamoja na kuepusha madhara yanayotokana na ufahamu mdogo juu ya afya zao.

Amesisitiza kuwa, endapo mradi wa TULONGE AFYA utafanyika vizuri, unaweza kusaidia kuimarisha  afya za wananchi, bila kutumia gharama kubwa na kuahidi kutoa ushirikiano kwa shirika hilo ili wananchi waweze kupata elimu hiyo ya afya, itakayoleta mabadiliko chanya kwenye jamii yao.

Akizungumza wakati wa kutambulisha mradi huo, mratibu wa mradi, Gervas Mollel, amesema kuwa lengo la mradi wa TULONGE AFYA ni kuwajengea wananchi uwezo kuwa na tabia chanya za afya ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha kina mama wajawazito na wenzi wao kuhudhuria Kliniki mapema na kupata huduma na ushauri muhimu wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua na zaidi kuwahimiza kujifungulia katika vituo vya afya na sio kwa wakunga wa jadi.

Kuwahamasisha vijana miaka 15-24 juu ya afya ya uzazi na kufanya maamuzi sahihi kabla ya  kuingia kwenye mahusiano ya  ngono au ya ndoa ikiwa na lengo la kujikinga na maambukizi ya magonjwa, mimba na ndoa za utotoni.

"Vijana wengi katika umri huu wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi, mimba za utotoni zisizo tarajiwa na athari nyingine juu ya afya zao, zinazofifisha na kuua ndoto zao na kupoteza dira ya maisha yao" amesema Mollel

Mollel amethibitisha kuwa TULONGE AFYA umejikita zaidi kwenye mambo manne ambayo ni  pamoja na Afya ya Uzazi, maambukizi ya VVU na UKIMWI,  ugonjwa Malaria na  Kifua Kikuu.

Hata hivyo viongozi hao wa jamii, wamekiri ukosefu wa elimu ya kutosha kwa jamii juj ya Afya na kuongeza kuwa kuna umuhimu wa jamii yao kupata elimu hiyo kwa njia rahisi na isiyo rasmi.

Naye Afisa Afya wilaya Issa Msumari, amesema kuwa, mradi huo wa TULONGE  AFYA, unategemea kutekelezwa kwa muda wa miezi saba, kwenye kata zote 27 za halmashauri ya Arusha kwa ushirikiano mkubwa wa watalamu wa ngazi ya wilaya, kata na vijiji na viongozo wa jamii wa ngazi zote za kata na vijiji na kuwafikia wananchi wote walengwa wa mradi huo ndani ya halmashauri hiyo.

Kikao kazi hicho, kimewakutanisha waheshimiwa madiwani wa kata zote 27, maafisa Watendaji wa kata zote, maafisa Afya wa kata zote na wataalamu wa afya ngazi ya halmashauri.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.