• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA NDOTO IN ACTION LAKABIDHI MSAADA WA VYUMBA VYA MADARASA SHULE YA MSINGI MARURANI

Posted on: December 14th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika la Ndoto in Action limekamilisha na kukabidhi mradi wa uboreshaji miundombinu ya shule ya msingi Marurani kata ya Nduruma  halmsahuri ya Arusha, mradi uliogharimu shilingi milioni 118.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mradi huo, iliyofanyika shuleni hapo, mkurugenzi wa shirika la Ndoto in Action, Hussein Salim, amesema kuwa, shirika hilo linashirikiana na serikali katika kuboresha huduma za jamii nchini, katika sekta za elimu, afya na ustawi wa jamii shuleni, na kuongeza kuwa wamefanikiwa kuboresha miundo mbinu ya shule ya msingi Marurani pamoja na kuwajengea uwezo wanafunzi katika nyanja ya afya ya hedhi kwa wasichana.

Ameongeza kuwa ndoto in Action, imefanikiwa kujenga na kukabidhi jumla ya vyumba 4 vya madarasa, madawati 120, matundu 10 ya vyoo vya wasichana na sehemu ya kujihifadhi wakati wahedhi, mfumo wa kuvuna maji ya mvua wenye matenki 8 yenye uwezo wa kuhifadhi lita elfu 4 za maji, pamoja na  miundombinu ya kunawia mikono.

"Shirika limewiwa kujenga choo cha wasichana chenye miundombinu ya maji na sehemu za kubadilishia taulo za kike kipindi cha hedhi lengo likiwa kuwoandolea wasichana changamoto ya kushindwa kuhudhuria masomo wakati wa hedhi, takwimu zinaonyesha zinaonesha, mtoto wa kike hushindwa kuhudhuria vipindi 3-4 kwa mwezi, vipindi 48 kwa mwaka wakati wa hedhi" ameweka wazi Mkurugenzi huyo wa Ndoto in Action.

Hata hivyo mkurugenzi Salim, amekubali ombi lililotolewa na uongozi wa shule hiyo ya Marurani la kukarabati vyumba vyote vya madarasa shuleni hapo, na kusema kuwa shirika linaanda mipango ya kutekeleza mradi huo wa kukarabati madarsa yote ya shule hiyo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kulishukuru shirika hilo kwa  kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita, amewataka walimu na wanafunzi kutumia miundombinu hiyo vizuri ili kuoandisha taaluma ya wanafunzi shuleni hapo.

"Tunaamini mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia yapo, kazi kwenu walimu na wanafunzi, kuongeza juhudi katika tendo la kujifunza na kufundisha ili lengo la serikali la kutoa elimu bora kwa wanafunzi wote litimie, wasichana mmewezeshwa kuwa na eneo la kujisitiri wakati wa hedhi, jambo ambalo litaongeza mahudhurio yenu shuleni, fanyeni jitihada katika masomo ili ufaulu wenu ulingane na mazingira bora mliyoandaliwa" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Aidha Mkurugenzi Msumi, ameupongez mpango wa kujenga mfumo wa kuvuna maji ya mvuo, unaokwenda sambamba na miundombinu ya kunawia mikono, miundombinu itakayowawezesha jamii ya Marurani kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, ikiwa ni mpango wa maendeleo dhidi ya UVIKO 19. 

Naye Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, mheshimwa Ojung'u Salekwa, ameushukuru hongozi wa shirika la Ndoto in Action na kusema kuwa mradi huo ni mkubwa na wa thamani katika sekta ya elimu ndani ya halmasahuri ya Arusha, na kuwataka kuendelea kutoa huduma hiyo kwa shule nyingine zenye mahitajimkama hayo.

Shule ya msingi Marurani ni miongoni mwa shule kongwe nchini ilianzishwa rasmi mwaka 1975, kutokana na kujengwa muda mrefu, miundombinu ya shule hiyo imekuwa chakavu, hivgo serilaki na wadau inaendela kuboresha miundombinu ya shuoe hiyo, mpaka sasa shule ina jumla ya wanafunzi 406, wasichana 210 na wavulana 196.


Arusha DC

KaziInaendeleaa✍✍











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.