• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Shirika la SOS Ngaramtoni latoa msaada wa vifaa vyenye thamani ya milioni 54

Posted on: November 10th, 2018

Shirika lisilo la kiserikali la SOS lenye makazi yake eneo la Ngaramtoni, linalojulikana kama Kijiji cha Kulea Watoto SOS, limekabidhi msaada wa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 54 kwa ajili ya wananchi wa halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru.

Akizungumza wakati wa kukabidhi misaada hiyo, Mratibu wa Miradi ya kuimarisha familia, Shirika la SOS, Innocent Estomihi, amesema kuwa, shirika lao, limejikita zaidi kuzijengea uwezo jamii zisizo na uwezo, katika ngazi ya familia ili zipate uwezo wa kujitegemea na kujipatia kipato, ambacho kiwawezesha familia hizo kujiinua kiuchumi.

Amefafanua kuwa, licha ya kuwa shirika hilo limejikita kuwahudhumia watoto yatima na wale walio kwenye hatari ya kupoteza familia, lakini pia shirika hilo, linahudumia familia zisizo na uwezo pamoja na kutoa misaada kwenye taasisi za serikali katika maeneo ambayo familia wanazozihudumia zinalazimika kupata huduma katika taasisi hizo.

Aidha ameitaja misaada iliyokabidhiwa imelenga kwenye sekta ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii, na kutaja misaada uliolenga sekta ya Elimu ni pamoja na Kompyuta 22 zenye thamani ya shilingi milioni 19 zilizotolewa kwenye shule ya Msingi Lemanyata na Engalaoni, huku wakikabidhi seti tatu za mashine za kukoboa na kusaga nafaka kwa vikundi vitatu vya wajasiriamali zenye thamani ya shilingi milioni 19.

Wamekabidhi pia vifaa tiba kwenye vituo 4 vya kutolea huduma za Afya, ikiwa ni pamoja na vitanda 7, vitanda 3 vya kujifungulia ' Delivery bed' na vitanda 4 vya kufanyia uchunguzi 'Examination bed', vifaa 4 vya kuchemshia gozi ' Sterlizer' pamoja na kifaa 1 cha kupimia ' Microscope', vyote vimegharimu kiasi cha shilingi milioni 16.

Hata hivyo Estomihi amesema kuwa, shirika lao haliko mbali na kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano, iliyojikita katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa hali ya chini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera licha ya kulishukuru shirika la SOS kwa misaada hiyo inayoipunguzia kazi serikali amewataka wananchi wote waliokabidhiwa misaada hiyo kuwa wazalendo na kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili kupunguza na kuondoa kabisa changamoto zilizokuwa zinawakabili.

Amefafanua kuwa licha ya wahudumu wa Afya kukabiliwa na changamoto ya mazingira magumu ya kazi, amewasisitiza wahudumu hao kutumia vifaa hivyo, kuwahudumia wagonjwa na si vinginevyo na kuthibitisha kuwafuatilia kwa karibu na kuhakikisha, wahudumu hao watoa huduma bora kwa wagonjwa.

"Natambua mazingira magumu ya kazi, wekeni uzalendo mbele, tumieni vifaa hivi tulivyopewa kuwapatia wagonjwa huduma bora, tutaendelea kuwafuatilia na kuhakikisha kila mtalamu anatekeleza majukumu yake" amesema Dkt. Mahera

Awali Kijiji Kulelea Watoto - SOS Ngaramtoni kinajishughulisha na kuhudumia watoto waliopoteza wazazi na wale walio kwenye hatari ya kupoteza malezi, na kinahudumia familia 185 zinazoishi ndani ya kijijini na familia 15 zinazoishi nje ya kijiji kwenye familia zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.