• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA SOS LAIMARISHA FAMILIA 514 KIUCHUMI  ARUSHA DC

Posted on: January 2nd, 2023

Na Elinipa Lupembe

Shirika lisilo la kiserikali la SOS Children Village linalofanya shughuli zake ndani na nje ya halmashauri ya Arusha kupitia mradi wake wa Uimarishaji familia ulioanza kutekelezwa mwaka 2007 katika kata 11 umefanikiwa kuwezesha familia 514 kuimarika kiuchumi na kuweza kuimarisha ulinzi na usalama wa mtoto.


Aidha, mradi huo ambao umefikia tamati mwezi Disemba mwaka 2022 huku familia 346 zikiwa zimeweza kujitegemea kiuchumi ambapo ni sawa na asilimia 86 ya familia zilizokuwa zikinufaika na mradi huo


Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuhitimisha mradi huo iliyofanyika katika viwanja vya shirika hilo vilivyopo katika kata ya Oltrumet, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Arusha, Daniel Ngasikiwe amesema kuwa kuna kila sababu ya kulipongeza shirika hilo kwa kuwa kupitia mradi huo wamegusa maisha ya watanzania wengi hasa waliokuwa na hali ya uchumi duni.


“Tunatambua dhahiri kuwa endapo hakutakuwa na uchumi imara ndani ya familia inatoa mwanya wa vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto kufanyika katika familia husika, hivyo shirika la SOS kupitia mradi huu wamefanya jambo kubwa sana na la kipekee kwani familia hizi zinazohitimu leo zimeweza kujitegemea kiuchumi na tunaamini zitaenda kusaidia na familia zingine ambazo hazikubahatika kuwepo kwenye huu mradiKw


Kwa upande wake Mratibu wa mradi huo kutoka Shirika la SOS Children Village, Kaiza Sakafu, ameweka wazi kuwa wamekuwa wakifanya kazi na Jamii, familia na watoto wenye umri wa kuanzia miaka 0-17 pamoja na vijana huku lengo kubwa likiwa ni kuwezesha familia na jamii kutoa ulinzi na usalama ikiwa ni pamoja na kuwahudumia watoto na kuhakikisha wanaishi katika mazingiira mazuri na salama.


“Haikuwa kazi rahisi, tunaamini kile ambacho tumeweza kuwasaidia watakithamini na kukitunza na hatimaye waweze kuizisaidia na familia zingine zinazowazunguka”. Amesisitiza Sakafu huku akitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wadau kuendelea kutoa ushirikiano ili miradi mingie kama hiyo iweze kuifikia jamii nyingi zaidi na kuleta mafaniHata


Hata hivyo wanufaika wa Mradi huo wameonekana kujawa na furaha tele wakati wa hafla hiyo fupi ya kuhitimu na kulishukuru shirika hilo pamoja na wadau walioshirikiana na kusema kuwa mradi huo umekuwa na manufaa makubwa sana kwao kwani sasa wanaweza kujitegemea kwa kiasi kikubwa na kutoa malezi bora kwa familia Kabl


“Kabla ya kukutana na SOS, nilikuwa mama wa nyumbani nikiwa siwezi kujikimu na kitu chochote lakini baada ya kujiunga na mradi huu mwaka 2020 sasa ninaweza kujikimu kimaisha mimi pamoja na familia yangu kwa kuwa sasa ninajua kushona nguo za mitindo mbalimbali na tuna kikundi cha akina mama.” Alisema Zulfa Athuman ambaye ni mama wa watoto wawili kutoka kata ya Oloirien alipozungumza mara baada ya hafla hiyo kuahirishwa.


Awali, Shirika hilo linatekeleza miradi mingine ya kijamii kwa kuendelea kupanua wigo zaidi wa kuzifikia jamii nyingi katika maeneo tofauti tofauti katika Mkoa wa Arusha huku likijikita kufanya kazi na familia, watoto na jamii kwa ujumla.


ARUSHA DC

KaziInaendelea ✍






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.