• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA TUMAINI JIPYA - NEW HOPE, LAWAKUMBUKA WASICHANA SEKONDARI LENGIJAVE

Posted on: November 20th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika la Tumaini Jipya -New Hope Tanzania, limeendelea kuimarisha ulinzi na usalama wa mtoto na kuepusha ndoa na mimba za utotoni kwa kujenga bweni la kulala wasichana 80, shule ya sekondari Lengiave, kwa gharama ya shilingi milioni 100.6.

Akizungumza wakati alipotembekea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa bweni hilo, mkurugenzi wa shirika la Tumaini Jipya Louise Richardson, amesema kuwa, shirika lao limefikia uamuzi wa kujenga bweni la wasichana, kwa lengo la kuwawezesha wasichana wa Lengijave, kupata muda wa kujisomea na kutimiza ndoto zao, ndoto ambazo wasichana wengi walilazimika kuzikatiza, kutokana na ndoa na mimba za utotoni, zilizotokana na mila na desturi za jamii ya kimaasai.

Louise ambaye ni raia wa Uingereza, aliyewahi kuishi kijiji cha Lengiajve kama 'volunteer' ameweka wazi kuwa, kipindi alichoishi Lengijave, alijionea namna wasichana wanashindwa kufikia malengo na ndoto zao, kutokana na kukosa fursa ya kusoma na kukamilisha safari ya masomo yao, kutokana na mila lakini pia kukosa fursa za kujiendeleza kimasomo.

"Nimeishi Lengijave, nawapenda sana wananchi wa Lengijave, ni rafiki zangu, ninatambua changamoto zinazowakabili wanachi wa Lengijave hasa wanawake na wasichana, hivyo tumeona ni bema kutafuta mbinu za kuwawezesha watoto wa kike, kujikwamua kifkra, kwa kusoma katika mzazingira bora" ameweka wazi Louise.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, amelishukuru shirika la Tumaini Jipya kupitia mkurugenzi wake mama Louise, na kuweka wazi kuwa, halmashauri inathamani mchango wa ASAS hiyo, hasa kwa kutataua changamoto zinazowakabili watoto wa kike wanaotokea katika jamii za kifugaji, na kuahidi kuendela kushirikiana na shirika hilo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na ustawi wa jamii ya kitanzania.

Hata hivyo wanafunzi wa shule ya sekondari Lengijave, wamefurahishwa na uwepo wa bweni hilo la wasichana na kusema kuwa, bweni hilo litawawezesha wasichana kusoma kwa utulivu na kukabiliana na changamoto za ndoa na mimba za utotoni zilizokuwa zinawkabili wasichana wengi wa Lengijave.

Dayana Frank mwanafunzi wa kidato cha III, amesema kuwa ameona tofauti kubwa ya kusoma akiwa bweni na akiwa nyumbani, kwa kuwa licha ya kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni lakini pia mazingira ya nyumbani hayamuwezeshi mtoto wa kike kujisomea kutokana na kupangiwa kazi nyingi za nyumbani mara baada ya kutoka shuleni.

Naye mkuu wa shule ya sekondari Lengijave, mwalimu Sunday Joseph, amelishukuru shirika hilo kwa msaada huo adhimu, msaada ambao unategemewa kuleta mabadiliko chanya shuleni hapo, kwa kuongeza kasi ya ufaulu kwa wasichana pamoja na kupandisha taaluma ya shule.

"Mara nyingi, licha ya umbali mrefu anaotembea mwanafunzi kwenda na kurudi shuleni, lakini bado watoto wa kike hawapati nafasi ya kujisomea wawapo nyumbani, kutokana na kutumia muda mwingi kufanya kazi za nyumbani, lakini pia wanakuwa kwenye hatari ya kukatishwa masomo, kutokana na mazingira na mila na desturi, uwepo wa bweni, utawafanya kutulia na kuelekeza mawazo yao katika masomo, tofauti na kuishi nyumbani" amesisitiza mkuu huyo wa shule.

Mkuu huyo wa shule amesema kuwa, tayari bweni hilo limeanza kutumika kama kambi, kwa wasichana wa kidato cha nne, wanaoendelea na mtihani wao wa Taifa kidato cha IV, 2021.

Awali shule ya sekondari ya Lengijave, ina jumla ya wanafunzi 387, wasichana 240 na wavulana 147, huku karibu asilimia 30 ya wanafunzi wa shule, wakikadiriwa kutembe umabali wa takribari Kilomita 10 mpaka 15  kwenda na kurudi shuleni.



#TUMAINI JIPYA - NEW HOPE - KaziInaendelaa..✍✍✍

#ARUSHA DC - KaziInaendelea...✍✍✍

#LENGIJAVE - KaziInaendela....✍✍✍










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.