• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA WaterAid LABORESHA MIUNDOMBINU YA MAJI VYOONI SHULE 8 ZA MSINGI ARUSHA DC UJENZI WA MIUND

Posted on: May 6th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Shirika la kimataifa la WaterAid Tanzania kwa kushirikiana na halmashauri ya Arusha, wamekamilisha utekelezaji wa mradi wa ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya tabia chanya za Afya, kwenye shule nane za msingi katika halmashauri ya Arusha.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Saad Mtambule amethibitisha kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huo, kwa shule nane za msingi, mradi uliogharimu  kiasi cha shilingi milioni 105, kufuatia fedha za ufadhili wa Idara ya Maendeleo ya nchini Uingereza - DFID na kutekelezwa na shirika la WaterAid Tanzania.Licha ya kuwashukuru wafadhili wa mradi huo,.

Mkurugenzi Mtambule, ameweka wazi kuwa, mradi huo umefanyika wakati muafaka, kutokana na ukweli kwamba shule za serikali katika halmashauri hiyo, zinao uhitaji mkubwa wa miundombinu bora ya vyoo na sehemu za kunawia mikono, kutokana na ongezeko la idadi kubwa ya wanafunzi, wanoandikishwa katika shule hizo tangu utekelezaji wa elimu bila malipo ya mwaka 2015, na kuanza raami mwaka 2016.

Ameongeza kuwa, uwepo wa miundombinu bora ya kunawia mikono shuleni, utawajengea uwezo wanafunzi kufahamu umuhimu wa kunawa mikono kwa nyakati tano muhimu pamoja na kuwa na tabia chanya za afya katika umri mdogo pamoja na kuwawezesha kujikinga na magonjwa yanayotokana na uchafu unaoshikwa kwa mikono.

Naye Mratibu wa Mradi WaterAid Arusha na Manyara, Upendo Muntambo, amesema kuwa mradi huo wenye lengo la kuwafanya wanafunzi kuwa na tabia chanya za afya za kunawa mikono kwa nyakati zote muhimu, zaidi mara wanapotoka chooni huku wakiendelea kuchukua tahadhari ya magonjwa ya kuhara, homa za matumbo, kipindipindu pamoaja na gonjwa hatari la Corona.

"Shirika la WaterAid kwa ufadhili wa DFID, limeona kuna umuhimu wa kuboresha miundombinu ya vyoo na sehemu za kunawia mikono kwenye shule za msingi,  lengo likiwa ni  kuwajengea  wanafunzi tabia ya kunawa mikono mara kwa mara ili kujikinga na maradhi yanayotokana na uchafu wanaoushika kwa mikaono yao" amesema Mratibu huyoNao

Nao wajumbe wa Kamati za shule hizo nane, wamelishukuru shirika la WaterAid kwa kuona umuhimu wa kuboresha  vyoo na miundombinu ya maji shuleni, kwani tatizo lilikuwa ni kubwa na lina hatarisha afya za watoto wao wawapo shuleni.Mwenyekiti wa Kamati ya shule ya Msingi Olosiva, Stevene Songoyo, amesema kuwa uwepo wa vyoo bora vyenye miundo mbinu bora ya kunawia mikono shuleni, utawakinga wanafunzi kupata magonjwa yanayotokana na uchafu ikiwemo homa za matumbo, kuharisha pamoja na gonjwa hatari la Corona.

Hata hivyo Afisa Afya, halmashauri ya Arusha, Issa Msumari amesema  kuwa, ujenzi wa miundombinu hiyo,umeambatana na utoaji elimu na uanzishwaji wa klabu za usafi katika shule hizo, klabu ambazo zitasimamia utunzaji wa miundimbinu pamoja na wanafunzi hao kuelemishana juu ya umuhimu wa unawaji mikono mara baada ya kutoka chooni sambamba na kufuatilia mwenendo wa matumizi ya miundombinu hiyo kwa usimamizi wa walimu wa Afya katial shule hizo.

Aidha utekelezaji wa mradi huo, umehusisha ukarabati wa vyoo na miundombinu ya maji, ujenzi wa sehemu za kunawia mikono,  kampeni ya kuhamasisha tabia chanya za afya pamoja nanuanzishwaji wa Klabu za Afya kwenye shule zote zilizopata mradi huo, ikiwa ni pamoja na shule ya msingi Olosiva, Mringa, Seliani, Olmotonyi, Lemanyata, Leminyoro, Oldonyosambu na shule mpya ya  Enaboishu Academy.











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.