Na Elinipa Lupembe.
Katika kilele cha Siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia, halmashauri ya Arusha, imefanya kikao kazi cha tathmini ya matukio ya ukatili wa kijinsia huku takwimu zikionyesha watoto wakiume wakiwa kwenye hatari kubwa ya kufanyiwa ulawiti.
Katika kikao hicho watoto walipata fursa ya kuelezea namna Klabu zao zinavyowawezesha kujitambua na jinsi ya kujikinga na kukaniliana na matukio ya ukatili hususani ulawiti kwa watoto wa kiume pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo katika kuelemishana wao kwa wao.
Watoto hao wamesema kuwa kupitia klabu hizo, wamejengewa uwezo na wameweza kutumia maarifa hayo kuelemisha wenzao shule na nyumbani pia, mafanikio ambayo yameanza kuwafanya watoto wa kiume kuanza kutambua hali halisi ya ulawiti unaoendelea kwenye jamii.
Hata hivyo wamebainisha baadhi ya changamoto zinazowakabili watoto ni pamoja na wazazi kukosa muda wa kukaa na watoto wao, mila na desturi pamoja familia kuwaamini ndugu, jamaa na marafiki, watu ambao ndio wanaowafanyia watoto ukatili huo.
Awali katika kikao kazi hicho, kimefanikiwa kuweka malengo ya utekelezaji wa kupambana na matukio ya kingono dhidi ya watoto na kukubaliana kuwalinda watoto wate na sio watoto wa kike peke yao.
Kikao kazi hicho kilichowakutanisha viongozi wa klabu za watoto wa kiume 'Boys Vac Lab' shule sita za msingi, walimu walezi wa klabu hizo, wanasheria, mawakili, Polisi Dawati la jinsi pamoja na watalamu wa Halmashauri hiyo.
Halmashauri kwa kushirikiana na shirika la CWCD inatekeleza mradi wa kwanza wa kupinga ukatili wa kingono kwa watoto wa kiume, kupitia klabu za 'Boys Vac Lab' kwenye shule sita za msingi kwa ufadhili wa Foundation for Civil Society.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
PPCHA ZA MATUKIO KATIKA KIKAO KAZI CHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.