• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YADHAMIRIA KUTOKOMEZA VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO KATA YA BWAWANI...

Posted on: September 8th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Kufuatia mkakati wa serikali ya awamu ya sita wa kutokomeza vifo vya wanawake na watoto wakati wa kujifungua kwa kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati na kila kata inakuwa na kituo cha afya, umefanyika kwa vitendo kwenye kata ya Bwawani halmashauri ya Arusha, kwa serikali kutoa shilingi milioni 357 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Bwawani, kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo kata ya Bwawani, Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda Mtaifikolo, amethibitisha serikali kutimiza lengo la kutokomeza vifo vya kina mama na watoto wakati wa kujifungua kwa vijiji vyote vinne vya kata hiyo kuwa na zahanati huku  sasa ikiendelea na ujenzi wa kituo kipya cha Afya Bwawani.

Amesema kuwa kutokana na Jiografia ya kata ya Bwawani, uwepo wa vituo vya kutolea huduma za afya ndani ya maeneo yao ni muhimu sana kwa kuwa licha ya kuwarahisishia upatikanaji wa huduma muhimu za afya, itaondoa vifo visivyo vya lazima  hususani kwa kina mama na watoto wakati wa kujifungua na wananchi wote kupata huduma za afya katika maeneo yao.

"Tunaishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kushusha fedha nyingi za utekelezaji wa miradi kwenye kata hii ya Bwawani, wananchi watanufaika na miradi hii, kutokana na ukweli kuwa walipata adha kubwa ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za afya, jambo ambalo kwa sasa litakuwa historia kwao" Amesema Mkuu huyo wa wilaya.

Hata hivyo wananchi wa kata ya Bwawani wamemshukuru pia Mhe. Rais kwa kuwajali na kuona umuhimu wa kuwapa fedha za kujenga kituo cha afya, mradi ambao haujawahi kutokea tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika.

Farida Msuya mkazi wa kijii cha Bwawani, ameweka wazi kuwa, kukamilika kwa kutuo hicho kutawaondolea adha wananchi hasa wanawake wajawazito, wanapopata changamoto wakati wa kujifungua na kulazimika kufuata huduma za afya Kituo cha afya cha Nduruma au mjini Arusha.

"Tunamshukuru mama Samia, tunamuombea kwa Mungu kwa kutuonea huruma na kutujengea kituo cha afya, kipindi cha nyuma wapo kinamama wenzetu walipoteza watoto na wengine maisha kwa kujifungulia nyumbani na wengine kuchelewa kupata huduma kutokana na umbali, kwa sasa tunaamini hakuna mama atajifungulia nyumbani na hakutakuwa na vifo visivyokuwa vya lazima" Amesema Esta Supatoi

JONAS Laiza, ameelezea matumaini makubwa ya kituo hicho kuwa, kitawasaidia wananchi kupata huduma ambazo hazikupatikani kwenye zahanati, kuna watoto wanaozaliwa kabla ya siku, huwa kwenye hatari kubwa ya kupoteza maisha wanapozaliwa kwenye zahanati, uwepo wa kituo cha afya utaokoa maisha ya watoto hao.

Awali Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi,  amefafanua kuwa mradi huo unatekelezwa kwa shilingi milioni 357 ukijumuisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) milioni 143.7, milioni 121.2 wodi ya wazazi,  na milioni 92.1 ujenzi wa nyumba ya watumishi yenye uwezo wa kuishi familia tatu (3 in 1), ujenzi uko kwenye hatua ya kupaua na unategemea kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba 2023.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.