• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YAWEZESHA KAYA KUANZISHA VIKUNDI VYA KUWEKA NA KUKOPA

Posted on: September 29th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF, kupitia Mpango wa Kunusuru kaya Masikini, umekuwa na programu ya wanufaika wa mpango kuunda vikundi vya kuweka, kuwekeza na kukopa lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa  kujiinua kiuchumi kupitia vikundi hivyo.

Kama ilivyo kawaida ya vikundi vingine vya kuweka na kukopa, wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini kijiji cha Mungushi kata ya Bwawani, wamefanikiwa kuwa na kikundi imara kilichoanza miaka mitatu iliyopita.

Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kukutana na wanakikundi hao, siku ya malipo ya ruzuku ya mwezi 7/8, na kuzungumza na wanufaika hao, ambao wameweka bayana kuwa, walianzisha kikundi chenye jumla ya wanakikundi 15 na kukipa jina la CHIPUKIZI GROUP, kikundi ambacho kimewawezesha kuongeza kipato cha kaya, kinachowawezesha kumudu kupata mahitaji muhimu ya kaya zao.

Katibu wa kikundi cha CHIPUKIZI, Grace Sayale, amesema kuwa walipata mafunzo ya uundaji wa vikundi vya kuweka, kuwekeza na kukopa kutoka kwa wawezeshaji wa TASAF, na kuamua kujiunga kwenye kikundi na kuanza kuweka fedha na kukopeshana kwa riba ya asilimia 5 na hukutana kila wakati wa malipo ya ruzuku ya TASAF.

Aidha Grace ameishukuru Serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha kifedha, kwa kuwa hapo awali maisha yalikuwa magumu kwao na familia zao, kwa sasa kina mama wengi wameamka kiakili na kifkra, kila mwanamke anapambana kuwa na shughuli inakayomuingizia kipato tofauti na zamani.

"Kikundi kimetusaidia kukutana na kubadilishana mawazo ya kimaendeleo, wamama wengi wameamka na hata wasio walengwa wa TASAF, wanafanya kazi za kuingiza kipato, hakuna mwanamke siku hizi ana muda wa kupiga umbeya, zaidi tunajivunia kuwa na Rais mwanamke naye ametufanya tujiamini zaidi" Amefafanua Grace

Naye Mweka Hazina wa Kikundi cha CHIPUKIZI, Paulina Thomas, amefafanua kuwa, wao kama wanakikundi wana malengo ya kufika mbali kiuchumi, hivyo wanatumia pesa za ruzuku wanazipata kupitia TASAF kuweka na kukopa na kufanyia miradi midogomidogo ya ujasiriamali, kilimo na ufugaji.

"Tumewekeana mikakati kabla ya kumkopesha mwanakikundi, tunahakikisha ana malengo na kutuchanganulia matumizi ya fedha hiyo na mipango ya urejeshaji, ili mtu asikope pesa bila malengo" Amefafanua Mweka Hazina Paulina

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini, unaendelea kutekeza miradi mbalimbali, lengo likiwa ni kwejengea uwezo wanakaya wa kujikimu kimaisha, unaokwenda sambama na maendeleo ya kijamii katika sekta za afya, elimi na uchumi wa kaya.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍


PICHA ZA KIKUNDI CHA CHIPUKIZI SIKU YA KUWEKEZA



Wanakikundi cha Chipukizi Group' wakiwa kwenye shughuli za kikundi za kukusanya pesa ya wekeza kwenye ofisi ya kikiji cha Mungushi mara baada ya kupokea ruzuku ya fedha za TASAF kwa mwezi 7/8 2022


Wanakikundi wa Chipkizi group wakikusanya fedha za kuwekeza.




Katibu wa Kikundi cha Chipukizi Grace Sayale ( wa kwanza kushoto) akiweka akiandika muhitasari kwa ajili ya kumbukumbu za kikundi na Mweka Hazina wa Kikundi Paulina Thomas (wa kwanza kulia) akihesabu fedha za makusanya ya kikundi.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.