• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF YAZIDI KUBORESHA AFYA ZA WANAFUNZI SHULENI, KUPITIA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI

Posted on: April 23rd, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Wananchi wanaonufaika na fedha za ruzuku za mpango wa kunusuru kaya masikini, mpango unaotekelezwa na Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Jamii - TASAF, wamekiri fedha hizo kuwanufaisha katika kupunguza makali ya maisha pamoja na kujikwamuua kiuchumi na kijamii, huku fedha hizo zikiwawezesha wazazi wengi wenye watoto wanaosoma shule za kutwa, kulipia gharama za chakula cha mchana..

Wanakaya hao wa kijiji cha Ekenywa kata ya Olturumet, halmashauri ya Arusha, walio kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini, wameyasema hayo walipozungumza na mwandishi wetu, wakati wa zoezi la kupokea fedha hizo za ruzuku kwa kipindi cha miezi miwili ya Januari na Februari 2021, malipo yaliyofanyika kwenye shule ya msingi Ekenywa.

Wamesema kuwa, licha ya kuzitumia fedha hizo kujipatia mahitaji muhimu ya nyumbani na kuanzisha miradi midogo midogo, fedha hzio pia zimewawezesha kuwalipia watoto wao chakula cha mchana shuleni, kwa kuwa watoto wao wanasoma shule ambazo, wanatakiwa kuchangia chakula cha mchana kulingana na sera ya elimu ya mwaka 2015.

Martha Loishiye Mollel, mnufaika wa Mpango wa kunusu kaya maaikini, mama anayelea wajukuu wawili, ameekiri kuwa pindi anapopokea pesa za TASAF, licha ya kuzitumia kwa matumizi ya nyumbani, pesa hizo pia huzitumia kuwalipia wajukuu zake pesa za chakula cha mchana shuleni kama sera ya elimu inavyoelekeza.

"Kama wazazi tunatakiwa kuwalipia watoto wetu chakula cha mchana wawapo shule, pesa nilizopokea leo, nimetumia kiasi kidogo kuwalipia wajukuu zangu  chakula cha mchana, nanafurahi kwa kuwa nilikiwa na deni, nilikuwa nadaiwa shilingi elfu 15, leo mnimelipa, sasa wajukuu zangu watasoma kwa amani". Amesisitiza Martha.

Naye Mariam Peter, mwanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Osiligi, amesema kuwa kaya yao hupokea fedha za ruzuku ya TASAF na mara nyingi huzitumia kununulia chakula pamoja kununua mahitaji yao ya shule, lakini pia hutumia kwa kulipia chakula cha mchana shuleni.

"Sisi tupo watoto watatu, mama yetu ni mgonjwa na baba anaishi nchini Kenya, huja nyumbani mara chache, pesa hizi zinatusaidia sana, nikipokea huwa tunanunua chakula, na pesa hizi nilizopkea leo nitamalizia kulipa fedha ya chakula shuleni, kukamilisha deni la muhula wa kwanza ambao tunalipa shilingi elfu 50 kwa muhula". Amefafanua Mariam.

Hata hivyo mwenyekiti wa Kitongoji cha Ekenywa, mheshimiwa Wilson Piniel Mollel, amesema kuwa kijiji chake kina kaya 482 zilizo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini, ameishukuru serikali kupitia mradi wa TASAF kwa kuwa ruzuku hiyo, licha ya kuwawezesha wananchi wake kujikwamua kiuchumi, kwa kujipatia  mahitaji ya muhimu lakini pia  kaya hizo maskini, zimeweza kumudu kuwalipia watoto wao walioko shuleni chakula cha mchana na kuwafanya watoto hao kusoma kwa amani na utulivu na kuongeza kuwa kama sio TASAF watoto wengi wangeshindwa kupata chakula cha mchana.

Mwalimu wa chakula,  shule ya msingi Ekenywa, mwalimu Ema Mashana, amethibitisha kuwa wazazi wanopekea fedha za TASAF, huwalipia watoto wao chakula cha mchana wawapo shuleni, na mara nyingi pindi wanapopokea fedha hizo hulipa, na kwa kuwa malipo hufanyikia shuleni hapo, inakuwa rahisi wao kutoa fehda hizo.

Aidha amefafanua kuwa, wazazi kupiti Kamati ya shule walikubaliana kila mzazi kuchangia sado 5 za mahindi na sado 2 za maharagwe sado 2 kwa mwaka, (kipimo kisischo rasmi) na kwa wazazi wasiokuwa na mazao hayo hulazimika kulipia kiasi cha shilingi 10 kwa ajili ya  maharagwe na shilingi efu 11 kwa mahindi kwa mwaka.

Awalii halmashauri ya Arusha, imepokea fedha kiasi cha shilingi milion 319, kutoka serikali kuu kupitia Mfuko wa Taifa wa Maendelo ya Jamii -TASAF,  mradi wa Mpango wa Kunusu Kaya masikini, ikiwa ni fedha za ruzuku kwa kaya masikini, kwa kipindi cha mwezi Januari na Februari, 2021, huku jumla ya kaya 8,167 zikunufaika na fedha hizo, kutoka vijiji 45 vya halmashauri hiyo.












Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.