• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TEA YAONDOA MSONGAMANO WA WANAFUNZI MADARASANI, SEKONDARI SOKON II

Posted on: February 17th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.


Katika kuboresha miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia kwenye shule za sekondari za kata, serikali kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania - TEA, imekamilisha ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa, viti na meza 150, shule ya sekondari Sokon II, halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi shuleni hapo, mkuu wa shule sekondari Sokon II, mwalimu Prisca Mbele, ameweka wazi kuwa, kukamilika kwa vyumba hivyo vya madarasa, kumeondoa msongamano wa wanafunzi darasani na kuwezesha shule hiyo, kufikia malengo ya  wastani wa  wanafunzi 50, kukaa ndani ya chumba kimoja cha darasa, jambo ambalo limefanikisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia shuleni hapo.


Aidha Mkuu huyo wa shule amesema kuwa, ujenzi wa vyumba hivyo 3 vya madarasa umegharama kiasi cha shilingi milioni 60 kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania na kuongeza kuwa, licha ya kuondoa upungufu wa vyumba vya madarasa zaidi umeondoa msongamano wa wanafunzi madarani, na umewezesha shule hiyo kufikia mpango wa uwiano wa wanafunzi 50 kwa darasa moja.


"Tunaishukuru serikali kwa kuweka nguvu kubwa kuboresha miundombinu ya shule yetu, shule haina umri mkubwa tangu ianzishwe mwaka 2015, lakini ina miundombinu inayojitosheleza, tuna madarasa ya kutosha, shule ina vyumba 27 vya madarasa , maabara 3 za masomo ya Sayansi, maabara ya somo la ICT, ofisi za walimu, tuna jumla ya wanafunzi 978  wanaotumia vyumba 20 vya madarasa" amefafanua Mkuu huyo wa shule.


Naye mwalimu wa Taaluma shuleni hapo, mwalimu Geofrey John amesema kuwa, utoshelevu wa vyumba vya madarasa shuleni hapo, unawezesha walimu kuwafikia wanafunzi wote wakati wa kufundisha, jambo ambalo wanaamini litaimarisha kiwango cha taluma na kupandisha ufaulu shuleni hapo.

Hata hivyo mwalimu huyo wa taaluma, ameweka wazi, kuendelea kuimarika kwa ufaulu shuleni hapo, katika mitihani ya Taifa na kufikia 97.4 % kwa matokeo ya kidato cha nne, na  99.4% kwa matokeo ya kidato cha pili kwa mwaka 2021.


Denning Innocent mwanafunzi wa kidato cha pili, amethibitisha wanafunzi wote kufurahishwa na uwepo wa madarasa ya kutosha shuleni kwao, na kuthibitisha kuwa kunawapa nafasi ya kujifunza katika mazingira mazuri, na pia kunawaongezea ari ya kujifunza.


"Tunaishukuru serikali kwa kutujengea majengo mazuri shuleni kwetu, kwa sasa tunasoma kwenye mazingira mazuri,mhatuna tofauti na shule za 'private', kila mwanafunzi anakaa kwenye meza na kiti chake, nafasi ni kubwa darasani, tuna maabara za masomo yote ya Sayansi, tuna chumba cha ICT, hii inatupa moyo wa kusoma kwa bidii na kufaulu mitihani yetu ya Taifa" amesisitiza mwanafunzi Denning


Awali shule ya sekondari Sokon II, kata ya Kiutu ni miongoni mwa shule za kata inayokuwa kwa kasi kubwa, iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2015 huku Serikali kwa kushirikiana na wadau wa elimu ikiweka nguvu kubwa za kuhakikisha shule hiyo inakua kwa kasi na kutimiza ndogo za wazazi walioanzisha shule hiyo. 


ARUSHA DC

#KaziInaendelea✍✍✍

#elimubilamalipo

#mamlakayaelimutanzania



Wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Sokon II wakiwa darasani .

 Hali ya chumba cha darqsa 



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.