• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TRC YAKUSUDIA KUJENGA RELI YA KISASA (SGR) KWA MIKOA YA KANDA YA KASKAZINI

Posted on: March 26th, 2025

TRC YAKUSUDIA KUJENGA RELI YA KISASA (SGR) KWA MIKOA YA KANDA YA KASKAZINI.


(Jumanne, Machi 25, 2025 – Arusha)


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Bw. Masanja Kadogosa ofisini kwake kuhusu mpango wa ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway) itakayounganisha mikoa ya Kanda ya Kaskazini.


Katika kikao hicho, Bw. Kadogosa alieleza kuwa Serikali inatarajia kuanza mchakato wa ujenzi wa reli hiyo, mradi unaotekelezwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kama sehemu ya maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Ujenzi huu unalenga kuboresha miundombinu ya usafirishaji na kukuza uchumi wa Mikoa ya Kanda ya Kaskazini na mikoa jirani.


Akizungumza kuhusu manufaa ya mradi huo, Bw. Kadogosa alisema kuwa reli hiyo ya kisasa itakuwa chachu ya maendeleo kwa mikoa ya kanda ya kaskazini Arusha ukiwa mmoja wapo hasa katika sekta ya uchukuzi, usafirishaji,Utalii, biashara na madini. Alifafanua kuwa uwepo wa madini ya Magadi soda eneo la Engaruka na bonde la Ziwa Natron katika mkoa wa Arusha imekuwa chachu ya ujenzi wa mradi huo, huku akibainisha kuwa machimbo ya madini hayo yana uwezo wa kudumu kwa zaidi ya miaka mia moja.

Aidha, alieleza kuwa ujio wa bomba la mafuta kutoka Hoima- Uganda hadi Chongoreani-Tanga utahitaji mfumo madhubuti wa usafirishaji wa mafuta ghafi, na reli hii itakuwa njia mojawapo muhimu ya kusafirisha mafuta hayo hadi masoko ya mataifa mengine katika Afrika.


Kwa upande wake, Mhe. Makonda alimshukuru Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa unaofanyika katika Mkoa wa Arusha, akiahidi kuwa wakazi wa mkoa huo wataendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazoletwa na serikali ya awamu ya sita.

Pia, Makonda alisisitiza kuwa Arusha imejipanga kuweka rekodi kwa idadi kubwa ya kura kwa Rais Samia katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu kama ishara ya shukrani kwa miradi inayotekelezwa, ikiwemo ukuzaji wa uchumi, uimarishaji wa sekta ya utalii, madini, na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara.

Ikumbukwe kuwa Nchi jirani ya Kenya kwa miaka mingi inatekeleza mradi mkubwa wa uchimbaji,uzalishaji na usafirishaji wa madini ya magadi soda

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.