• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ubalozi wa Japani wachangia milioni 195 za ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Sokon II

Posted on: March 22nd, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Ubalozi wa Japani nchini Tanzania, umetoa kiasi cha dola za kimarekani 87,974 ikiwa ni takribani shilingi  milioni 195 za kitanzanis, kwa ajili ya ujenzi wa jengo la ghorofa lenye vyumba vinne vya madarasa na samani zake, kwenye shule ya sekondari Sokon II halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru.

Hata hivyo, tayari Murugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera amesaini mkataba  na balozi wa Japani nchini Tanzania Balozi, Shinishi Goto, katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa balozi huyo mapema wiki iliyopita.

Akizungumza wakati hafla hiyo, Balozi wa Japani, amesema kuwa, serikali ya Japani inashirikiana vema na serikali ya Tanzania, na inaona umuhimu wa kuunga mkono sera ya serilikali ya Tanzania ya kutoa elimu bila malipo kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne,  sera inayotekelezwa kwa kasi na kwa vitendo na serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, amefafanua kuwa, kiasi hicho cha fedha, kilichotolewa na ubalozi wa Japani, kitawezesha ujenzi wa msingi wa ghorofa moja yenye vyumba 12 vya madarasaa, na kuwezesha kukamilisha msingi wa jengo hilo la ghorofa moja na kukamilisha vyumba vinne vya madarasa pamoja na samani za madarasa hayo kati ya vyumba 12 vya jengo zima.

Mkurugenzi Mahera, ameongeza kuwa, ukamilishaji wa miundombinu vyumba 12 vya madarasa vya shule hiyo, unahitaji kiasi cha shilingi milioni 330.2, ambapo kiasi cha shilingi milioni 90 kitatolewa na serikali kupitia wizara ya Elimu na shilingi milioni 50 zitatolewa na halmashauri kupitia mapato yake ya ndani.

" Ili kukamilisha jengo lenye vyumba 12 vya madarasa, tunahitaji shilingi milioni 330.2, hiyo serikali itashirikiana na ubalozi wa Japani kukamilisha ujenzi wa mradi huo" amesema Dkt. Mahera.

Mkuu wa shule ya sekondari Sokon II, mwalimu Mwamvita Kilonzo, amethibitisha uwepo wa changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa shuleni hapo, usiowiana na idadi kubwa ya wanafunzi waliosajiliwa shuleni hapi.

Amefafanua kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 1,006, ikiwa na vyumba 11 vya madarasa, kukiwa na uhitaji wa vyumba vingine 11 ili kufikia vyumba 22 ambavyo vitawiana na idadi ya wanafunzi.

Mhandisi wa Ujenzi, halmashauri ya Arusha, mhandisi Bibie Manzi, amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo, uko katika hatua za awali ambapo mchakato wa kumpata mkandarasi umeshapatikana, na ujenzi unategemea kuanza mapema mwezi ujao wa Aprili na unategemea kukamilika mwishonj mwa mwaka huu wa 2019.


Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera (kushoto) na Balozi wa Japani nchini  Tanzania Balozi Shinishi Goto (kulia) wakinyoosha juu mkataba wa milioni 195, mara baada ya kusaini kusaidia  ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya sekondari Sokon II.


Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, wakisaini mkataba na Balozi wa Japani nchini Tanzania, Balozi Shinishi Goto, nyumbanj kwa Balozi huyo.

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, akizungumza wakati wa utiaji saini mkataba na Balozi wa Japani nchini Tanzania, nyumbani kwa Balozi huyo.

Picha ya pamoja ya wajumbe waliohudhuria utiaji wa saini ya mkataba na Balozi wa Japani nchini Tanzania, Balozi Shinishi Goto, nyumbani kwa Balozi huyo.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.