Wananchi wa kata ya Nduruma halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru wamefurahia neema ya uendelezwaji na upanuzi wa miundombinu ya kituo cha Afya cha Nduruma ambacho kimepatiwa fedha za kukamilisha hadhi ya kituo hicho cha Afya.
Afisa Mipango halmashauri ya Arusha Anastazia Tutuba amesema kuwa serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kufanya upanuzi wa miundo mbinu ya kituo hicho ili kiwe na hadhi kufuatia vigezo vya wizara ya Afya.
Amesema kuwa fedha hizo zitatumika kujenga maabara, jengo la upasuaji, nyumba ya kuhifadhia maiti, Kliniki ya mama na mtoto, sehemu ya kuchomea taka pamoja na nyumba ya mganga.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.