Na Elinipa Lupembe
Halmashauri ya Arusha inaendelea na usimamizi wa utekelezaji wa miradi mikubwa mitatu inayotekelezwa na fedha za kutoka Serikali kuu kupitia profram ya kuboresha miundombinu ya shule za serkondari (SEQUIP) shilingi bilioni 1.4.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo, Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu halmashauri ya Arusha Anna Urio, ameitaja miradi inayotekelezwa na fedha hizo kuwa ni apamoja na ujenzi wa shuoe mpya ya sekondari kata ya Moivo milioni 587.4, ujenzi wa mabweni na ukarabati shule ya sekondari Mringa milioni 360 na ujenzi wa nyumba ya walimu yenye sehemu mbili (2 in 1) shule ya sekondari Kiutu shilingi milioni 90.
Afisa Mipango huyo licha ya kuishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi hiyo mikubwa, amesema kuwa kukamilika kwa mradi hiyo kutatimiza adhma ya serikali ya kuwa na miundombinu bora ya shule kwa kuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia kwa walimu na wanafunzi pamoja na kutawapunguzia wanafunzi adha ya kutembea umbali mrefu kwenda shuleni.
Aidha ameuzungumzia mradi wa shule mpya ya sekondari kata ya Moivo kuwa utajumuisha ujenzi wa jengo la Utawala, vyumba 8 vya Madarasa, Maabara 3 za Sayansi, chumba cha TEHAMA, Maktaba, matundu ya vyoo vya wasichana na wavulana na chumba maalum cha wanafunzi wenye ulemavu, kichomea taka 1, mnara wa tank la maji lenye ujazo wa lita zaidi ya elfu 20
Awali Mirradi wa shule mpya ya sekondari kata ya Moivo umefikia hatua ya kumwaga jamvi kwenye majengo yote 6, mradi unaogharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 584.
PICHA ZA MAENDELEO YA UJENZI
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.