• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Vikundi vya wanawake na vijana wajasiriamali waaswa kutumia fedha za mikopo kwa malengo waliyoyakusudia

Posted on: February 26th, 2018

Vikundi vya Wanawake na Vijana wajasiriamali halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru, wameaswa kutumia fedha za mkopo walizopewa kwa malengo waliyoyakusudia wakati wa kuomba mkopo ili kuwarahisishia urejeshaji wa fedha walizokopa. 

Akizungumza kwa niaba ya wanawake wenzie wakati wa kukabidhiwa mfano wa hundi mwenyekiti wa kikundi cha JADEKI kilichopo kata ya Kiranyi kinachojishughulisha na usindikaji mvinyo ndugu Juliana Mamuya amewaasa wanawake wenzie kuhakikisha fedha walizopewa wanazitumia kwenye biashara halisi walizozikusudia na kuziandika kwenye mchanganuo waliowasilisha wakati wa kuomba mkopo. 

Mamuya amethibitisha kuwa kuna baadhi ya wanawake ambao baada ya kukabidhiwa fedha wanabadili mawazo ya biashara walizozikusudia kuziifanya na kuamua kuanzisha biashara nyingine tofauti jambo ambalo linasababisha kushindwa kurejesha fedha hizo kutokana na ugeni wa biashara wanazokurupuka nazo. 

"Unakuta mwanamke ni mfugaji wa kuku anaomba mkopo kuongeza mradi wa kuku lakini akipokea pesa anaingiwa na tamaa na kununua toyo, siku mbili toyo imeibiwa mara imepata ajali ni dhahiri mtu huyu hawezi kufanya marejesho kwa wakati na kuingia kwenye mgogoro yeye na familia yake" amesema Mamuya 

Amewaasa wanawake wenzake kuacha tamaa badala yake kusimamia biashara zao walizozoea kuzifanya kila siku jambo ambalo litawainua kiuchumi na kuwarahisishia urejeshaji wa fedha walizozikopa . 

Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mheshimiwa Idd Kimanta, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera amewataka wanawake hao kijikita kwenye shughuli zao za uzalishaji utakaowawezesha kurejesha fedha na kupata fursa ya kuchukua mikopo mingine na zaidi kutoa nafasi kwa makundi mengine kupewa mkopo. 

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mheshimiwa Noah Lembris amewataka wanawake hao kutambua kuwa fedha hizo zinatokana na kodi mbalimbali wanazolipa na kurudishiwa asilimia kumi ya mapato hayo na kuwataka kutumia fedha hizo kujikwamua kiuchumi na kurejesha kwa wakati kwa kuwa mkopo sio zawadi. 

Hata hivyo Afisa Maendeleo ya Jamii halmashauri ya Arusha Angela Mvaa amewataka wanawake na vijana kujikita zaidi kwenye uanzishaji wa viwanda vidogo na uzalishaji wa malighafi za viwanda ili kuwenda sambamba na sera ya serikali ya viwanda.

Ameongeza kuwa kwa sasa serikali itajikita zaidi kutoa mikopo kwa wajasiriamali wenye kujishughulisha na viwanda vidogo pamoja na uzalishaji wa malighafi za viwanda. Aidha amesisitiza kuwa lengo la kutoa mikopo hiyo ni kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa kuwawezesha wananchi kujiajiri kuelekea uchumi wa kati ifikapo 2020. 

Halmashauri ya Arusha imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 220 kwa vikundi 43 vya wajasiriamalii, ikiwemo vikundi 38 vya wanawake na vikundi 5 vya vijana, fedha hizo ni asilimia 10% ya fedha za mapato ya ndani ya halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA August 14, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA BW. SELEMAN MSUMI AWASHONEA SARE MADEREVA WA HALMASHAURI HIYO

    October 02, 2025
  • WIZARA YA KILIMO KUPITIA MAMLAKA YA UDHIBITI WA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO (COPRA) YAZINDUA RASMI MSIMU WA UNUNUZI WA ZAO LA PARACHICHI KWA MWAKA 2025/2026

    September 27, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ARUMERU MWINYI AHMED MWINYI AHITIMISHA MAFUNZO YA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT)

    September 21, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA AWAASA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA USAFI

    September 21, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.