• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WAWAKILISHI WA WANANCHI ARUSHA DC WAISHUKURU SERIKALI KUJENGA MADARASA 100

Posted on: December 4th, 2021

Viongozi wawakilishi wa wananchi halmashauri ya Arusha, wameishukuru  serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mheshimiwwa Rais mama Samia Suluhu Hassani kwa kuwajengea vyumba 100 vya madarasa kwa wakati mmoja, katika shule 2 za msingi shikizi na shule 30 za sekondari, kwa ajili ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2022, jambo ambalo wamekiri kuwapunguzi mzigo wa michango wanachi wao.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, kwenye maeneo yao, maeneo ambayo ujenzi wa vyumba vya madarasa ya mpango wa mapambano dhidi ya UVIKO 19 unaendeleo, viongozi hao hawakusita kushuru na kuipongeza serikali ya awamu ya sita, kwa mrari  huo mkubwa wa ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa, unaoendelea kutekelezwa kwenye shule za halmashauri ya Arusha kwa wakati mmoja, jambo ambalo wanakiri kuwa halijawahi kutokea katika awamu zilizotangulia.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Arumeru, Simon Saning'o, amesema kuwa CCM kama wasimamizi wa Ilani, wanashuhudia namna serikali ya awamu ya sita inavyotekeleza Ilani yake kwa vitendo katika maeneo yote Arumeru na nchi nzima, huku ikiwapunguzia wananchi wanyonge, mzigo wa michango ya ujenzi wa madarasa, ambao hufanyika kila mwaka ifikapo mwisho wa mwaka kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza.

"Kujengwa madarasa 100 kwa wakati mmoja ni historia katika halmashauri yetu, haijawahi kutokea, sisi kama wasimamizi wa Ilani tunashuhudia kasi ya ujenzi wa madarasa ambayo, yanaleta matumaini ya kukamilika kwa wakati na tunayomatumaini wanafunzi wote waliochagulia kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2022, wataingia wote kwa pamoja darasani tofauti na miaka ya nyuma ambapo wanafunzi walianza form one kwa awamu mbili huku wengine wakisubiri 'second selection', wanafunzi mbao huanza masomo kwa kuchelewa pia" amesema Mwenyekiti Saning'o.

Makamu Mwenyekiti halamshauri ya Arusha, na Diwani wa kata ya Matevesi, Mheshimiwa Freddy Mollel amesema kuwa, serikali ya awamu ya sita, imefanya mabadiliko makubwa katika kuwekeza kwenye miundo mbinu ya shule, jambo ambalo limewapa amani wananchi ambao kipindi hiki huwa wanahangaika kuchangishana na kujenga madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza. 

"Wananchi wamefarijika sana na ujenzi wa madarasa unaondelwa katika maeneo mengi, kwa ajili ya kidato cha kwanza, kwa kuwa miezi kama hii, huwa ni nyakati za kushikana mashati na wananchi vijijini ili kujenga madarasa ya Form one, lakini sasa serikali imewapumzisha wananchi na shughuli hizo za ujenzi wa madarasa ya kidato cha kwanza, hata wananchi wetu kwa sasa wana amani na wanaipongeza serikali yao.Amesema Makamu Mwenyekiti huyo.

Naye Diwani wa Kata ya Oloireni Mheshimiwa Erick Semboja, amesema kuwa wananchi wa eneo lake wanaipongeza serikali kwa kuwapunguzia mzigo wa kuchangia ujenzi wa madarasa ya kidato cha kwanza kwa mwaka huu, kwa kuwa kila mwaka huwa kunakuwa na uhitaji wa madarasa kwa mwaka unaofuata.

"Serikali imefanya jambo kubwa sana ambalo, limewapa wananchi kupumzika na michango ya vyumba vya madarasa, kupitia miradi hii wananchi wamejenga imani kunwa kwa serikali yao," amesema Mheshimiwa Erick Semboja.

Julius Mollel mkazi wa Olosiva (57), ameweka wazi kuwa, haijawahi kutokea katika shule yao ya Kiranyi, kujengwa madarasa 13 kwa wakati mmoja na kukamilika ndani ya miezi miwili ama mitatu, mara nyingi huwa tunajenga madarasa mawili ama matatu kwa shida sana, kwa kuchangishana pesa yetu ndogo na wakati mwingine madarasa hayo hushindwa kukamilika kwa ukosefu wa fedha, miezi kama hii hata viongozi wetu wamepumzika pai, maana ndio walikuwa wanahamasisha michango ya ujenzi na kuongeza kuwa  mwaka huu watasherehekea sikukuu ya Krismass na mwkaa mpya kwa utulivu.

Halmashauri ya Arusha inajenga jumla ya vyumba 100 vya madarasa, madarasa 96 sekondari na madarasa 4 kwa shule mbili shikizi kwa gharama ya shilingi bilioni 2,  fedha za mkopo wenye riba nafuu kutoka Benki ya Dunia, ikiwa ni mradi wa Mpango wa Maendeleo na Ustawi wa Taifa wa Mapambano dhidi ya UVIKO 19.


ARUSHA DC 

#KaziInaendelea✍✍






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.