VITUO VYA VILIVYOTEULIWA KUTOA CHANJO YA UVIKO 19, KATIKA HALMASHAURI YA ARUSHA.
1. KITUO CHA AFYA NDURUMA - KATA YA NDURUMA
2. ZAHANATI YA NGORBOB - KATA YA MATEVESI
3. HOSPITALI YA WILAYA YA OLTURUMET - OLTURUMET.
Serikali inategemea kuanza kitoa chanjo dhidi ya ugonjwa wa virus vya Corona kwa makundi yanayolengwa kuanzia tarehe 3, Agosti 2021, siku ya Jumanne, katika vituo 550 vya kutolea huduma katika mikoa yote ya Tanzania bara.
Aidha kutokana na Mwongozo wa Chanjo wa Taifa dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO, kufuatia Shirika la Afya Duniani (WHO), maelekezo ya COVAX FACILITY na upungufu wa uzalishaji wa chanjo toka viwandani, Chanjo hizi kwa sasa zinatolewa kwa kufuata vipaumbele vya makundi yenye uhitaji mkubwa ambayo ni (1) Watumishi wa sekta ya Afya, (2) watu wazima umri wa miaka 50 na kuendelea na (3) watu wenye magonjwa.
Hata hivyo Serikali imekuwa ikieleza, uchanjaji kwa makundi hayo yote nchini ni wa hiari au huru kwa kila mwananchi. Serikali imeelekeza kuwa chanjo hiyo ya COVAX FACILTY itatolewa bure na kupiga marufuku Hospitali yoyote (ya umma au binafsi) kulipisha Wananchi gharama yoyote katika zoezi hili la chanjo na kusisistiza kuwa zoezi hilo lifanyike kwa uadilifu na kwa haki kwa walengwa wa sasa.
Pamoja na Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kufanikisha upatikanaji wa chanjo nchini na kuanza kuchanja Wananchi, Wizara ya afya inaendelea kuwashauri Wananchi kuendelea kujikinga na UVIKO-19 kwa kunawa mikono, kuvaa barakoa, kukaa umbali za mita moja au zaidi, kuepuka misongamano na kufanya mazoezi.
* imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya*
CHUKUA TAHADHARI CORONA INAUA!
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.