Na. Elinipa Lupembe.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Salihi Geraruma, amewataka vijana kuwacha tabia ya kulalamika maisha magumu, badala yake kujishughulisha kwa kufanya kazi kwa bidii, sambamba na kutumia fursa uwezeshwaji kupitia ya asilimia 4 ya mikopo isiyo na riba, inayotolewa na halmashauri zenu.
Kiongozi huyo, amesema hayo wakati Mwenge wa Uhuru ulipotembelea Kikundi cha Vijana cha Winner Stunna, wanaojishughulisha na ufundi selemala na kupewa mkopo wa shilingi milioni 10 kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ya Arusha.
Licha ya kuwapongeza vijana amewasisitiza kufanya kazi kwa bidii, ili waweze kurejesha mkopo huo, ikiwa ni pamoja na kutengenza bidhaa zenye ubora ili kukabiliana na ushindani wa soko, ikiwa ni pamoja na kutafuta kazi zinazotolewa na serikali.
Hata hivyo ameuagiza watalamu wa halmashuri hiyo, kuwa karibu na vijana hao kwa kuwawezesha kupata kazi zinazotolewa na halmashauri ikiwe kuwa na mashine ya risiti ya mlipa kodi kutoka TRA 'EFD'.
"Wasaidieni vijana hawa kupata mashine ya EFD ili muweze kuwapa kazi kwenye halmashauri jambo ambalo litawawezesha biashara yao kukua, kuwakopesa tu haitoshi, lazima mbinu zaidi za kufanya biashara"
Mwenge wa Uhuru 2022, wenye kauli mbiu ya Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo, Shiriki kuhesabiwa Tuyafikie Maendeleo.
MWENGE WA UHURU Hoyeeeee
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.