• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali yagawa dawa za kuoshea mifugo kwa wafugaji Arusha DC

Posted on: January 29th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Wafugaji katika halmashauri ya Arusha wamepata neema ya mgao wa za viuatilifu vya kuua dawa ya kuogeshea mifugo ikiwa ni viuatilifu vya kuua vya kuulia wadudu aina ya kupe, mgao huo ni kufuatia mpango wa Serikali ya awamu ya tano wenye lengo la kuhamasisha wafugaji kuogesha mifugo yao, ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Wafugaji hao wamepata neema hiyo baada ya Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kutoa jumla ya lita sabini na tano (75) za viuatilifu aina ya 'Paranex' yenye kiini cha 'Alphacypermethtrin yenye uwezo wa kuua wadudu ya kupe kwa ajiki ya wafugaji wa vijiji vitano vya halmashauri ya Arusha.

Akizungumza wakati wa kukabidhi dawa hizo kwa wajumbe wa kamati za uendeshaji majosho za vijiji vinne, zoezi lililofanyika kwenye ofisi za Mifugo makao makuu halmashauri ya Arusha ,  Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo,  Dkt. Wilson Mahera, amewataka wajumbe hao kwenda kuhamasisha wananchi kuogesha mifugo yao, ili kuzuia vifo vya mifugo vinavyotokana na magonjwa yenezwayo na kupe na mbung'o.

Ameongoza kuwa, tafiti zinaonyesha kuwa, asilimia 72% ya vifo vya mifugo nchini, hutokana na magonjwa mbalimbali ikiwemo magonjwa yanayotokana na kupe na ndorobo, na kulisababishia taifa hasara ya takribani bilioni 63 kwa mwaka, huku takribani asilimia 70% ndama wanaozaliwa hufa kila mwaka, hii ni kutokana na wafugaji kukosa mwamko wa kuogesha mifugo yao.

Ili kuzuia vifo hivyo na hasara kubwa inayoligharimu taifa, serikali imeanza kuwawezesha wafugaji kwa kutoa dawa za kuogeshea mifugo ili  kuzuia magonjwa yanayoenezwa na kupe pamoja na kuhamasisha wafugaji kuogesha ng'ombe kupitia majosho yaliyo katika maeneo yao.

"Inaonekana wafugaji hawana mwamko wa kuosha mifugo yao, lakini kupitia serikali ya kijiji na  ninyi wajumbe wa kamati za uendeshaji majosho, hamasisheni wafugaji na simamieni vizuri zoezi hili ili kila mfugaji aweze kunufaika na huduma hiyo" amesema Mkurugenzi Mahera.

Aidha mkurugenzi Mahera, amewataka wajumbe wa kamati  hizo kushirikiana na serikali ya kijiji chini ya usimamizi wa maafisa mifugo wa ngazi zote, kusimamia vema utoaji wa huduma hiyo kwa wafugaji kwa kuhamasisha na kuwahimiza wafugaji kuogesha mifugo yao,  pamoja na kusimamia fedha za mapato na matumizi ili mradi huo uwe endelevu.

" Serikali imewapa dawa hizi ni kama mtaji wa kuanzia kutoa huduma ya kuogesha mifugo yenu,  mapato yatakayopatikana, yatumike kuendeleza huduma hii kwa wafugaji katika maeneo yenu, shirikianeni na serikali ya kijiji , na zaidi watumieni maafisa mifugo katika maeneo yenu, kupata ushauri wa kitalamu".  Amesisitiza Dkt. Mahera.

Naye Daktari wa mifugo, halmashauri ya Arusha, Dkt. Linus Prosper,ametaja bei elekezi iliyotolewa na  serikali  ya kuendesha huduma hiyo ya kuogesha mifugo, kwa kufafanua kuwa, bei ya ng'ombe mmoja kwa muosho mmoja ni shilingi 50 na shilingi 10 kwa mbuzi na kondoo kwa muosho mmoja.

Hata hivyo serikali imefafanua kuwa gharama hizo zinaweza kubadilika, kulingana na gharama halisi za uendeshaji wa josho katika eneo husika kutegemea maamuzi ya Kamati ya Uendeshaji wa Josho husika.

Aidha Dkt. Linus amezitaja kamati nne za majosho, zilizokabidhiwa dawa  kuogesha mifugo ni pamoja na Kamati ya Josho la Engutukoit kata ya Oldonyowas, Oloitushula kata ya Musa, kidali na Engalaoni kata ya Mwandet huku kila Josho likipata lita 10 za dawa.

Hata hivyo wajumbe wa kamati hizo wameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuwakumbuka wafugaji, kwani kwa miaka mingi sasa, serikali ilikua kama imewasahau na kuahidi kwenda kuhamasisha wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao,  kwa gharama nafuu ambazo hapo awali wafugaji wengi walikua wanashindwa kuzimudu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Josho la Oloitushula kata ya Musa, Manase Meoki, licha ya kuishuru serikali kwa kuwakumbuka wafugaji, amesema kuwa uwepo wa dawa hizo, zilizotolewa na serikali utawasaidia kupunguza gharama kubwa walizokuwa wakizitumia pamoja na kuepuka kuuziwa dawa zisizofaa na kuwataka wananchi wenzake kuunga mkona jitihada hizi za serikali.

Halmashauri ya Arusha ina jumla ya majosho 18, majosho  nane  kati ya hayo ndio yanatoa huduma, majosho matano hayatoi huduma kutokana na uhalisia wa maeneo yalipo  tayari kumeshakuwa miji na kuwa katika makazi ya watu hivyo hayatumiki kwa sasa, huku majosho matano yakihitaji ukarabati kutokana na uchakavu uliotokana na kujengwa muda mrefu.


Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera akimkabidhi mmoja wa mjumbe wa kamati ya uendeshaji josho (jina halikuweza kupatikana) box lenye lita kumi za dawa.


Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Majosho, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa dawa za kuogeshea mifugo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.