• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WADAU ABERCROMBIE & KENT PHILANTROPY WAWAKUMBUKA WANAFUNZI KITENGO MAALUM SHULE YA MSINGI ILIBORU

Posted on: April 21st, 2021

Na. Eliniap Lupembe.

Wadau wa maendeleo wa shirika la ABERCROMBIE & KENT PHILANTROPY (A&K) linalofanya shughuli zake mkoani Arusha, limetambua adha wanayopata wanafunzi wenye ulemavu, wanaosoma  kwenye kitengo cha elimu maalum shule ya msingi Ilboru, halmashauri ya Arusha, kwa kukosa sehemu ya kulia chakula na kuamua kuwaondolea adha hiyo na kuwajengea Bwalo la chakula.

Wadau hao marafiki wa shule hiyo, licha ya kutoa misaada mingi katika kitengo hicho, wameanza ujenzi wa Bwalo la Chakula walilolipa jina la 'Dinning & Kitchen Project', mradi ambao unategemea kugharimu  kiasi cha shilingi milioni 54 mpaka kukamilika kwake, mapema mwishoni mwa mwaka huu.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ilboru mwalimu Ronald Mwende, amesema kuwa msaada huo wa ujenzi wa Bwalo la chakula, umekuja wakati wa muafaka  kutokana na changamoto inayowajabili wanafunzi hao, ya kukosa mahali rasmi pa kulia chakula huku kituo hicho kina jumla ya wanafunzi 106 ambao wote wanapata chakula cha mchana shuleni, wakati wengine 65 wako bweni wakipata huduma ya chakula kwa muda wote.

"Ninawashukuru  sana wafadhili wa  A& K, kwa kuona umuhimu wa kujenga Bwalo, uwepo wa Bwalo utawafanya watoto hawa kupata chakula eneo ambalo ni rasmi na salama kiafya na kiakili pia, kwa kuwa watoto wenye mahitaji maalumu wanahitaji ungalizi wa hali ya juu muda wote tofauti na watoto wengine, hapa shuleni". Amefafanua mwali Mwende.

Hata hivyo, Diwani wa kata ya Ilboru Mhe. Lembris Ngiremo, amesema kuwa, Bwalo hilo litaeleta mapinduzi katika kata hiyo licha ya kutumika kwa ajili ya kulia chakula wanafunzi wenye mahitaji maalumu,  lakini pia litatumika kama ukumbi zinapotekea warsha mbalimbali, kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa kata hiyo.

Aidha Diwani huyo, amewataka wadau mbalimbali kujitokeza kuungana na serikali kuendeleza miundombinu ya kitengo hicho cha Elimu maalumu, kutoka mwitikio mkubwa wa jamii na kupeleka watoto wao wenye ulemavu shule, jambo ambalo limesababisha ngezeko la watoto hao kuandikishwa shule,  kutokana na serikali  kuwapa fursa watoto wenye ulemavu kupata elimu kwa maendeleo ya taifa la Tanzania.

Naye Anastazia Pastori, mwanafunzi wa darasa la nne, mwenye ulemavu wa kusikia kwa mbali, amelishukuru shirika la A &K, kwa kujenga Bwalo la chakula na kusema kwamba, bwalo hilo ni muhimu sana kwao, kwa kuwa hawana sehemu maalumu ya kulia chakula.

Awali Anastazia, ameipongeza serikali kwa kuwajali watoto wenye ulemavu kwa kuwapa kiapaumbele kwenye masuala ya elimu na kuonheza kuwa yeye amefanikiwa kujua kusoma na kuandika kawaida pamoja na matumizi ya lugha ya Alama, lugha ambayo licha ya kumsaidia kimasomo inamuwezesha pia kuwasaidia watu wenye usonji.

"Nilianza kusoma Kitengo Maalum kwenye darasa la ufundi, baada ya kumudu stadi  tatu za kuandika, kusoma na kuhesabu, nimeweza kujiunga na  mfumo wa elimu ya kawaida na sasa niko darasa la nne, ninajiandaa na mtihani wa Taifa wa darasa la nne, nikiwa na wenzangu wasio na mahitaji maalumu, na ninahakika nitafanya vizuri" amesistiza Anastazia.Katika shule ya msingi Ilboru, 

Kitengo hicho cha Elimu Maalumu,  kilianza rasmi mwaka 2001  kikiwa na wanafunzi 6, mpaka sasa kitengo kina jumla ya wanafunzi 106, kikiwa na wanafunzi  viziwi, usonji, ulemavu wa  akili, ulemavu wa viungo na ulemavu wa ngozi (albinisim), huku wanafunzi 65 kati ya hao, wakiwa wanalala bweni 65, wavulana 45 na wasichana 40.




BWALO LA CHAKULA SHULE MSINGI ILBORU KITENGO MAALUM




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.