• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wadau wa Afya Arusha DC kufanya matembezi shirikishi kutafuta fedha za kuboresha huduma za afya

Posted on: October 11th, 2018

Wadau kutoka sekta binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya dini,  wanaojishughulisha na masuala ya afya ndani ya halmashauri ya Arusha, wameweka mkakati wa kushirikiana na halmashauri hiyo, kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya afya kwa sasa.             

Wadau hao wameweka mikakati hiyo, wakati wa kikao kazi cha mwaka cha 'Private Partinership Performance (PPP)', kikao  kilichojumuisha wadau wa afya na watalamu wa halmashauri ya Arusha, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.  

Wadau hao, wameazimia kwa pamoja kufanya  matembezi shirikishi yatakayojumuisha wadau mbalimbali na wananchi wa maeneo husika, ambayo yatafanyika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, ikiwemo zahanati na vituo vya  afya kwa lengo la  kutafuta fedha za kuatua changamoto zinazo ikabili sekta hiyo ya afya.            

Aidha wadau hao wameweka kipaumbele cha matembezi hayo, kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vilivyo kwenye , maeneo ya pembezoni mwa halmashauri hiyo, kwa kuwa huko ndiko kwenye changamoto kubwa, kulinganisha na maeneo ya mijini.  

Akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi hicho, kwa niaba ya mkurugenzi Mtendaji,  Afisa Rasilimali Watu, halmashauri ya Arusha Mohamed Mavura, amewataka wadau wote wa afya ndani ya halmashauri hiyo, kushiriki kikamilifu kuisaidia serikali kutatua changamoto zinazoikabili sekata ya afya, ili kuhakikisha wananchi wote, wanapata huduma muhimu za afya katika maeneo yao kuanzia kwenye zahanati ndani ya vijiji vyao.

Mavura ameongeza kuwa sekta ya afya inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo kimsingi kuna baadhi ya changamoto ambazo, serikali inahitaji wadau kushiriki bega kwa bega kuzitatua.

Aidha amewataka wadau hao kushiriki katika, upatikanaji wa vifaa vya kisasa vya kutolea huduma za afya pamoja na ujenzi wa miundo mbinu ya vituo vya afya, kwa kuwa mpaka sasa halmashauri ina upungufu wa zahanati 20 kutoka zahanati 47 zilizopo ili kukamilisha uwepo za zahanati katika vijiji vyote 67.

"Serikali imeandaa mazingira rafiki ya ushiriki wa wadau katika kutatua changamoto za huduma za afya, hivyo niwatake wadau, mwisho wa kikao kazi hiki, tuweke mikakati ya pamoja ya namna ya kuinua sekta ya afya ndani ya halmashauri yetu, kwa kuweka vipaumbele katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa maeneo ya pembezoni mwa mji" amesema Mavura.

Aidha Afisa Utumishi huyo, amethibitisha kuridhishwa na kazi kubwa inayoifanywa na wadau hao wa afya na kuwaomba kutochoka bali kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili waweze kuisaidia halmashauri na serikali kwa ujumla kutimiza malengo katika kuboresha sekta ya afya.

Naye Mganga Mkuu wa halmashauri ya Arusha  Dkt.Petro  Mboya amesema kuwa, licha ya changamoto zinazoikabili sekta ya afya, sekta hiyo imepata mafanikio makubwa kwa mwaka ulioisha, mafanikio yaliyotekelezwa na  serikali kwa kushirikiana na wadau wa afya, ikiwa ni pamoja na ongezeko la bajeti ya dawa kutoka shilingi milioni 764.9 mwaka uliopita wa 2017/2018 na kufikia shilingi milioni 861.2 kwa mwaka huu mpya wa fedha unaoendelea wa 2018/2019.

Aidha Dkt. Mboya ameongeza kuwa kwa,  upatikanaji wa dawa  muhimu katika vituo vya  kutolea huduma za afya umeimarika hadi kufikia asilimia 97, kuboreka kwa utoaji huduma za afya pamoja na kupunguza idadi ya vifo kwa mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Hata hivyo wadau waote walioshiriki kikao kazi hicho, wameupongeza uongozi wa halmashauri ya Arusha kwa ushirikiano mkubwa unaotolewa kwa  wadau hao na kuahidi kuendelea kushiriki kwa hali na mali kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya afya, huku wakisisitiza  kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli.    

Mdau kutoka shirika la  Engender Health, Sebastian Macrice, amethibitisha ushiriki wa shirika lao, katika kutatua changamoto kama zilivyowasilishwa na Idara ya afya, huku akiwataka watalamu wa afya kujitoa kwa moyo kuwahudumia wagonjwa licha ya changamoto zilizopo.

                           ................._________...........


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA KIKAO KAZI






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.