• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA MAENDELEO KUTOKA UJERUMANI WAUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI

Posted on: November 14th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wadau wa Maendeleo halmashauri ya Arusha, kutoka nchini Ujerumani, wameendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha miundombinu ya Afya, lengo likiwa ni kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii, hususani maeneo ya vijijini.

Wadau wa shirika la Help for Maasai Children kwa ufadhili wa marafiki kutoka nchini Ujerumani,  wamefanikisha mkakati huo wa serikali kwa kujenga nyumba ya mtumishi wa afya, yenye thamani ya shilingi milioni 30, kwenye zahanati ya Nameloki kijiji cha Losinoni juu Kata ya Oldongowas.

Akizungumza wakati wa kukabidhi nyumba hiyo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha, mwakilishi wa marafiki hao kutoka Ujerumani, Andreas Reinke, amesema kuwa, wamefikia hatua hiyo kwa kuona adha ya upatikanaji wa matibabu kwa wananchi wa Losinoni juu, na kuamua kujenga zahanati na sasa kujenga nyumba ya mtumishi ili wananchi wapate na  huduma za dharura hasa nyakati za usiku.

"Tulijenga zahanati, tukaona tujenge nyumba ya mtumishi, ili kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za afya kwa wepesi kwa wananchi wa Losinoni, tunaungana na serikali ya Tanzania, kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya unaimarika kwa wananchi wote". Amesema Andreas.

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kuwashukuru wadau hao amekiri kuthamini mchango huo mkubwa kwa wananchi, sambamba na kutekeleza vipaumbele vya serikali ikiwemo kusogeza huduma za afya kwa wanachi kwa lengo la kupunguza vifo vya wanawake na watoto nchini.

Aidha Mkurugenzi Msumi amewataka wananchi wa Losinoni Juu, kuutunza mradi huo pamoja na wahudumu wa afya waliopangiwa kufanya kazi hapo, ili udumu kwa sasa na vizazi vijavyo.

"Wananchi wa Losinoni Juu, mmepata zahanati, serikali imeleta madaktari hapa, hakikisheni mnatunza miundo mbinu na mali zote pamoja na kushirikiana na watumishi hawa, ni ndugu zenu, ni watanzania wenzetu". Amesistiza Mkurugenzi Msumi

Hata hivyo wananchi wa Losinoni juu wamekiri kufurahishwa na uwepo wa zahanati na nyumba ya daktari, kwa kuwa imewarahishishia upatikanaji wa huduma pindi wanapokuwa wagonjwa lakini zaidi kwa kina mama wajawazito na watoto.

Naishiye Lomutiye amebainisha kuwa wajawazito waliteseka sana na kulazimika kujifungulia nyumbani, jambo ambalo ilikuwa ni hatari kwa maisha ya mama na mtoto, kwa sasa hufuma zipo wajawazito watahudumiwa zahanati.

Naye Diwani wa kata ya Oldonyowas, licha ya kuwashukuru marafiki hao, ameipongeza serikali kwa kutoa wahudumu wa afya pamoja na vifaa tiba, vilivyofanikisha utoaji na upatikanaji wa matibabu kwa wananchi.

"Zahanati ilijengwa mwaka 2018, kwa juhudi za serikali mwaka huu tumepata daktari na wauguzi, serikali ya mama Samia inatuthamini sana, wananchi tuendelee kushirikiana na serikali kwa ajili ya maendeleo yetu na Taifa letu". Ameweka wazi Mhe. Kijana.

ARUSHA DC

#KaziIendelee✍✍✍



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.