• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAFANYABIASHARA NA WANANCHI WA NDURUMA WAISHUKURU SERIKALI KUANZISHA SOKO NA GULIO....

Posted on: August 26th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Wafanyabiashara na wananchi wa kata ya Nduruma wameishukuru serikali kwa kutoa eneo la kunzaisha soko la bidhaa za vyakula kijiji cha Samaria, soko ambalo litafanya kazi kila siku na siku moja ya gulio, ukiwa ni mpango wa serikali wa kutenga maeneo rasmi kwa ajili ya kufanyia biashara hususani kwa wafanyabiasha wadogowadogo.


Wananchi hao hususani wafanyabiashara,  wamebainisha hayo wakati wa uzinduzi wa soko hilo la Samaria, lililozinduliwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha Mhe. Dkt. Ojung'u Salekwa na kuweka wazi kuwa, walilisubiri soko hilo kwa muda mrefu na sasa serikali ya awamu ya sita imetimiza ndoto zao.


Licha ya kuishukuru serikali, wamethibitisha  uwepo wa soko hilo utawawezesha kinamama wa Nduruma kupata sehemu karibu ya kufanyia biashara kutokana na ukweli kuwa, eneo lao halikuwa na soko na kuwalazimu kwenda mbali kufanya biashara na wengine kufanyabiashara pembezoni mwa barabara, na kuipongeza serikali ya mama Samia kupitia serikali yao ya Kijiji kuona umuhimu wa kuwawekea soko ndani ya kata yao.


"Sisi kina mama tulikuwa tunaamka saa nane za usiku ili kuwahi kufika kwenye masoko ya Jiji la Arusha, tulienda soko la Kilombero au Tengeru ili kuleta bidhaa za kuuza kwenye magenge yetu, uwepo wa eneo la soko utatupunguzia kazi ya kwenda masoko ya mbali" Amesema mfanyabiashara Frida Ngolocho


Magdalena Hamadi, amewashukuru viongozi wa kata na kijiji kwa kuanzisha soko rasmi, kwa kuwa walitumia muda mwingi kwenda kufanya biashara mbali kufuata magulio maeneo mengine, sasamwemepata soko la kila siku nyumbani.


Naye Fatuma Mohamed, ambaye ndiye mwanzilishi wa soko hilo amebainisha serikali kuwatendea haki kwa kuweka soko, kuwagawia vizimba  na kuweka umeme utakaowawezesha kufanya biashara hadi usiku huku akiwataka viongozi kusimamia vizuri uendeshaji wa soko hilo na kuliboresha ili liwe kubwa zaidi na la kisasa kwa kuwa kuna eneo la kutosha.


"Tunaamini huu ni mwanzo mzuri, tunaiomba serikali kuendelea kuboresha miundo mbinu ya soko hili ili likue na liwe la kisasa zaidi, zaidi tunaomba uongozi wa soko kusimamia vema uendeshaji wa soko hili ili lisife kama ilivyo kwa masoko mengine na kuwasisitiza wafanyabiashara wote kuondoka kwenye maeneo yasiyo rasmi na kuhamia sokoni hapo" Amesema Fatuma


Hata hivyo Diwani wa kata ya Nduruma Mhe. Raymond Mollel, ameweka wazi furaha ya wananchi wa kata hiyo kutokana na kusubiri mchakato wa uanzishaji wa soko hilo uliyochukua miaka mingi, soko ambalo litahudumia kata zaidi ya tatu, kwa kuwa maeneo haya hayana soko karibu.


"Wananchi walilazimika kwenda soko la mjini Kilombero na Tangeru, jambo ambalo kwa sasa wafanyabiashara na wakulima watauza na kunua bidhaa zote hapa, lakini pia wapo kina mama waliofanyia biashara pembezoni mwa barabara,  ambayo ilikuwa ni hatari kwa maisha yao, lakini sasa wamepata soko rasmi". Amesisitiza Mhe. Diwani


Awali Soko la Samaria limezinduliwa rasmi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha Mhe. Dkt. Ojung'u Salekwa kwa kukata utepe na kuwataka wafanyabiashara wote kuondoka kwenye ameneo yasiyo rasmi na kufanyaia biashara zao sokoni, huku akiahidi kuendelwa kuboresha miundombinu ya soko hilo kadri fedha zitakavyopatikana.


ARUSHA DC  NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.