Na. Elinipa Lupembe.
Wajumbe wa Kamati ya fedha, Utawala na Mipango, wakikagua ujenzi Kituo kipya cha Afya cha Oloirieni kata ya Oloirieni, mradi unaogharimu kiasi cha shilingi milioni 450 fedha za mapato ya ndani kupitia fidia ya deni la Lakilaki.
Wajumbe hao wa kamati ya fedha licha ya kuridhishwa na ubora mradi huo, wakithibitisha ubora wa majengo unaoendana na thamani ya fedha 'value for money', wameshauri kuonheza kasi ya ujenzi ili mradi huo uweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma za afya kwa wananchi wa kata ya Oloirieni na kata za jirani.
Nao wananchi wa kata ya Oloirien, wameishukuru serikali yao ya awamu ya sita, inayoongozwa na Mama Samia Suluhu, kupitia uongozi wa halmashauri Arusha kwa kupeleka miradi ya zaidi ya shilingi milioni 650 kwa kipindi kifupi, miradi ambayo wamekiri haijawahi kutokea hapo awali.
"Tunaishukuru sana serikali ya awamu ya sita, kata ya Oloirieni haijawahi kupata miradi mikubwa yenye fedha nyingi kwa wakati mmoja, ndani ya miezi sita tumepata fedha za kutekeleza miadi mikubwa miwili, hii haijawahi kutokea tangu kata hii imenazishwa" wameshuhudia wananchi hao.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Oloirieni, mheshimiwa John Aminiel, ameishukuru serikali pia kwa mradi wa kituo cha afya, na kusema kuwa wananchi wa kitongoji chake wameamua kutoa kipande cha ardhi chenye ukubwa wa mita 20, ili kuonheza ukubwa wa eneo la kituo hicho kwa ajili ya kuongeza majengo ya wodi za wagonjwa ili kituo hicho kukidhi sifa.
Naye Afisa Mtendaji kata ya Oloirien Charles Sikoi, ameweka wazi kuwa kata ya Oloirieni, imepokea kiasi cha shilingi milioni 650, ikiwa shilingi milioni 450 fedha za fidia ya deni la lakilaki kwa ajili ya ujenzi wa Kituo kipya cha afya, pamoja na shilingi milioni 200 za ujenzi wa vyumba 10 vya madarasa shuke ya sekondari Mringa, zikiwa ni fedha za Mpango wa Taifa wa Mapambano dhidi ya UVIKO 19.
Sikoi ameongeza kuwa, wananchi wa Oloirieni wamefurahia ujenzi wa kituo hicho cha afya , na wanatamani kikamilike na kuanza kutoa huduma haraka, na kuongeza kuwa Kituo kinategemea kuhudumia takribani elfu 20 wa kata ya Oloirien na vitongoji vyake pamoja na watu wa vitongoji vya kata za jirani.
Ziara hiyo ya Kamati ya fedha ni ya kawaida yenye jukumu lamkukagua shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya halmasahuri kwa kila robo ya mwaka,myaani kila baada ya miezi mitatu.
ARUSHA DC#
KaziInaendelea ✍✍✍
PICHA ZA MATUKIO
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.