• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WAMETAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZA KISASA ZA KILIMO ILI KUONGEZA UZALISHAJI

Posted on: August 4th, 2020

Na Elinipa  Lupembe.  

Wakulima na wafugaji wadogo Kanda ya Kasazini, wametakiwa kubadili mitazamo na kuachana na kilimo cha mazoea badala yake, kuanza kutumia teknolojia mbalimbali za kilimo na ufugaji, zinazoelekezwa na watalamu, kwenye maonesho ya wakulima Nane Nane, ili kufanya kilimo cha kisasa, chenye kuzalisha mazao yenye tija kwa mkulima na taifa pia.
      Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Omari Mgumba, wakati akifungua shughuli za Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kaskazini, yanayoendelea kwenye Viwanja vya Themi eneo la Njiro, Jijini Arusha kuelekea maadhimisho ya  sikukuu ya Wakulima NANENANE mwaka 2020.
           Naibu Waziri huyo wa Kilimo, amewasisitiza wakulima na wafugaji kufanya kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia za kisasa, zinazomuwezesha mkulima mdogo kulima kisasa na kuzalisha mazao mengi na bora, kwa matumizi ya chakula na biashara kwa kujiongezea pato la familia, na kukuza uchumi wa wakulima na taifa.
        "Nimejionea teknolojia nyingi za kisasa kwenye Mabanda ya maonesho, teknolojia rahisi zenye uwezo wa kumfanya mkulima, kulima kisasa na kuzalisha mazao mengi yenye ubora, niwasihi watalamu wawezesheni wakulima na wafugaji wadogo kutumia teknolojia hizo na si kuishia kwenye viwanja hivi vya maonesho" amesisitiza Naibu Waziri Mgumba.
       Hata hivyo Naibu Waziri huyo, ameweka  wazi kuwa, tayari serikali imekamilisha uaandaji wa maghala na vihenge vya kuhifadhia mazao ya chakula kanda ya Kaskazini, maghala ambayo yatasaidia uhifadhi wa mazao ya wakulima, pindi watakapovuna, na kusubiri mpaka bei ya mazao itakapokuwa rafiki sambamba na kuhifadhi kwa ajili ya kuongezea thamani mazao hayo kwa matumizi ya viwanda vyetu nchini, lengo likiwa kumfanya mkulima kuacha kuuza mazao yake kwa bei ya kutupa kipindi cha mavuno.
       Aidha ameelezea matarajio ya serikali ya kufufua zao la ngano na shairi Kanda ya Kaskazini kwa kurejesha mashamba makubwa ya Basutu mkoani Manyara mikononi mwa serikali, mashamba amabayo yatagawiwa kwa  wakulima wazawa na wawekezaji wazawa, ili watanzania waweze kutumia mashamba hayo kujiongezea kipato kwa faida yao na maendeleo ya nchi yao.
       Naye mkuu wa mkoa wa Arusha Idd Kimanta amewasisitiza watalamu na taasisi zinazoshghulika na pembejeo za kilimo, kuwafuata wakulima shambani, na kuwafundisha matumizi ya teknolojia hizo pamoja na kuweka mipango rahisi kwa wakulima kumiliki teknolojia hizo na kuzitumia ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na kumkomboa mkulima mdogo wa kitanzania.
      "Kanda hii ya Kaskazini ina maeneo mengi ya kilimo yenye kuzalisha mazao ya nafaka na mbogamboga, wakulima wakiwezeshwa kutumia teknolojia za kisasa, wataondokana na kilimo kisicho na tija na kufanya kilimo biashara kwa maendeleo ya viwanda vyetu nchini" amesema Mkuu huyo wa Mkoa.
        Hata hivyo, licha ya changamoto zinazowakabili wakulima, baadhi ya wakulima  wameendelea kuishukuru serikali kwa kutambua mchango wao katika maendeleo ya taifa, pamoja na juhudi kubwa za kuwaunganisha wakulima na makampuni  zinazozalisha teknolojia za kilimo na taasisis za fedha, jambo ambalo linazidi kuwainua wakulima na kujikita kwenye kilimo cha kisasa, kilimo kinachowakomboa wakulima wengi kiuchumi kwa sasa, tofauti na miaka ya nyuma.
       Hild chondo, mkulima wa kijiji cha Kiseriani kata ya Mlangarini mkoani Arusha, amesema kuwa  licha ya kuishukuru serikali kwa kuwaunganisha wakulima wadogo na taasisi zinazotoa huduma za pembejeo na watalamu  wakilimo, bado wakulima wanakabiliwa na changamoto ya masoko ya mazao yao pindi wanapovuna kwa kuwa, mara nyingi bei inakuwa chini, kiasi cha wakulima wengi kuuza mazao yao kwa bei ya hasara.
         Maonesho ya Wakulima kuelekea maadhimisho ya Sikukuu za wakulima mwaka 2020, yanaendeleo kwenye Viwanja vya Themi eneo la Njiro, Jijini Arusha, yenye kauli mbiu isemayo: Kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora.

PICHA ZA MATUKIO KWENYE MAONESHO YA WAKULIMA NANENANE 2020 KANDA YA KASKAZINI.








Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.