• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKUU WA NCHI ZA EAC, SADIC WAKUTANA DAR ES SALAAM KULETA SULUHU DRC

Posted on: February 8th, 2025

Wakuu wa Nchi za EAC, SADC Wakutana Dar Kuleta Suluhu DRC.

Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wamekutana Jijini Dar es Salaam Nchini Tanzania, kutafuta suluhu ya mzozo Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) uliodumu kwa zaidi ya miongo miwili mpaka sasa.

Kikao hicho kilichowakutanisha wakuu tisa wa nchi za Jumuiya za EAC na SADC pamoja na wawakilishi wa nchi wanachama wa kanda hizo, kimeketi nchini Tanzania ambapo mwenyeji wa kikao hicho ni Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC.


Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Dkt. Samia amesema nchi za EAC na SADC hazipaswi kukaa kimya kwani zina wajibu wa kushughulikia mgogoro huo unagharimu watu wasio na hatia.

"Sote tunafahamu, DRC bado inakabiliwa na mgogoro, kama viongozi tutakaa kimya jambo hili sio zuri, nchi zetu zina wajibu wa kuhakikisha tunashughulikia changamoto hii ambayo inaathiri watu wasio na hatia, ni muhimu kutafuta suluhisho la kudumu, kama mtetezi wa amani, nchi yangu itaendelea kusaidia masuala ya kidiplomasia ili kumaliza mgogoro huu" amesema Rais Samia.


Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Watu wa Kenya, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe. William Ruto amesema mgogoro wa DRC haupaswi kushughulikiwa kwa mtutu wa bunduki bali kwa njia za mazungumzo kwa kusikilizana na kushauriana.


"Mgogoro huu hautaweza kusuluhishwa kwa njia za kijeshi, lazima tukatae kupiga mabomu, ni suluhu za kidiplomasia ndizo zinazohitajika, njia kama hiyo inahitaji kushirikisha wadau mbalimbali, mtakubaliana nami kuwa mazungumzo ya amani sio udhaifu bali ni kusikilizana na kushauriana" amesema Rais Ruto.


Rais Ruto amesema hatua za haraka zinahitajika kunusuru watu wa DRC.

"Tunaona gharama kubwa inayoikabili DRC, mamilioni ya watu wanahama, matishio ya vifo, watoto wanahusishwa katika vikosi vya majeshi, tunahitaji kuchukua hatua kwani usalama wa nchi hiyo unaathiri Dunia nzima na athari zake zinatakiwa zisipuuzwe" amesema Rais Ruto.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.