• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAARUSHA DC WAKO TAYARI KUHESABIWA 23.08.2022.

Posted on: August 19th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wananchi wa halmashauri ya Arusha, wamethibitisha utayari wao wa kuhesabiwa katika zoezi muhimu la kitaifa la Sensa ya watu na makazi, linalotegemewa kufanyika 23.08.2022.

Wananchi hao kwa makundi tofauti, wamedhihirisha utayari wao wakati wa matembezi ya hiari ya kuhamasisha zoezi hilo la Sensa ya watu na makazi, yaliyoandaliwa na halmashauri hiyo, matembezi yaliyoongozwa na Katibu Tawala wilaya ya Arumeru, Mwl. James Mchembe.

Wamesema kuwa kutokana na serikali kupitia mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan, kuhamasisha na kuelezea umuhimu wa umuhimu wa Sensa ya watu na makazi kupitia majukwaa mbalimbali, wananchi hao wamedhihirisha wazi kusubiri kwa hamu siku hiyo muhimu kwa watanzania na Taifa lao.

Athmana Idd (23) akiwakilisha vijana wa bodaboda eneo la kwa Idd, amesema kuwa serikali imejitahidi kuelezea umuhimu wa Sensa na wao kama vijana wako tayari kuhesabiwa huku wakiendelea kuhamasisha vijana wenzao na wananchi wote kuhesabiwa siku hiyo.

Nao wazee wa Ngaramtoni wamebainisha kuwa wako tayari kuhesabiwa na kuweka wazi kuwa hii sio sensa yao ya kwanza, wamekuwa wakihesabiwa kwa miaka mingi sasa hivyo wazee wengi wanaelewa sana umuhimu wa Sensa.

Mzee Lomayani Mollel (78) mkazi wa Lengijave, amesema kuwa  katika maisha yake amepata kuhesabiwa mara kadhaa na kuongeza kuwa zoezi la Sensa sio geni kwake, yeye na wazee wa umri wake, wengi wanafahamu umuhimu wa Sensa na wako tayari kuhesabiwa.

Naye mwakilishi wa waumini wa wakristo, Mchungaji  Charles Kingu, amesema kuwa, maandiko yatuambia  Sensa ilikuwepo tangu enzi za Kaisari Agusto, wakati Bwana Yesu anazaliwa, Bikira Maria na Yusufu walikwenda Bethlehem kuhesabiwa, hivyo wakristo wanafahamu umuhimu wa sensa na wako tayari kuhesabiwa.

"Tunaona wakati huo, watu walikwenda eneo moja kuhesabiwa, lakini serikali yetu imeandaa utaratibu wa makarani kutufuata katika kaya zetu, niwatake watanzania kuona zoezi hili rahisi sana kwetu, tunafuatwa nyumbani, basi sote tuwe tayari kuhesabiwa ili kufikia malengo ya Serikali" Amesisitiza mchungaji huyo

Muumini wa dini ya kiislam Shekhe Nuru Mkwazu, amesema kuwa hata dini ya kiislam, inaelezea umuhimu wa watu kuhesabiwa, hivyo kupitia maandiko ya Kuran Tukufu waumini wa dini ya kiislamu, wanelewa maana na umuhimu wa Sensa hivyo wako tayari kuhesabiwa.

Diwani wa kata ya Olturumet Mhe. Joseph Tinayo, naye amethibitisha kuwa, wananchi wa kata yake, wametambua na kuelewa umuhimu wa Sensa ya watu na makazi na wako tayari kuhesabiwa.

Awali Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mhe. Ojung'u Salekwa, amefafanuwa kuwa, wananchi wa halmashauri yake, wako tayari kuhesabiwa kutokana na umuhimu wa Sensa yenye lengo la kuweka Mipango ya maendeleo kulingana na idadi ya watu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya Arumeru, Katibu Tawala wilaya hiyo, Mwl. James Mchembe, ameweka wazi kuwa Sensa ya watu na makqzi ni suala la kitaifa lenye lengo la kupanga mipango ya maendeleo kulingana na idadi ya watu, ikiwa ni nguzo kuu ya kuoamabana na maadui ujinga, umasikini na maradhi kupitia takwimu sahihi zitakapatikana kupitia zoezi hilo la Sensa.

Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ndani ya halmashauri hiyo, imefanya matembezi ya hiari kuanzia eneo la kwaIdd mpaka Standi ya mabasi Ngaramtoni lengo likiwa ni  kuwahamasisha wananchi kushiriki zoezi la Sensa ya Watu na makazi 23.08.2022.


HAKIKISHA UMEHESABIWA 









Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.