Na Elinipa Lupembe
Wanafunzi wanaoishi kijiji cha Lemanda wanaosoma shule ya msingi Oldonyosambu wamemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule ya msingi kijijini kwao, shule ambayo itaondoa changamoto ya watoto hao kutembea umbali mrefu.
Wanafunzi hao wamesema kuwa wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya Kilomita 15 kwenda na kurudi shuleni kila siki jambo ambalo licha ya kusababisha changamoto za kimwili na kisaoikolojia linasababisha pia baadhi ya watoto kuacha shule kwa kujata tamaa ya kuendelea na masomo.
Zawadi Simon wanafunzi wa darasa la 6 shule ya msingi Oldonyosmabu amemshukuru mama Samia kwa kujenga shule ya msingi kijiji cha Lemanda, shule ambayo itawaondoelea changamoto ya kutembea umbali mrefu na kuwapa nafasi ya kusoma kwa bidii.
"Tunamshukuru sana Mama Samaia atatusaidi kusoma karibu na nyumbani, tunatembea umbali mrefu kutoka Lemanda mpaka shuleni, tunafika shuleni tumechoka sana na tunarudi nyumbani tumechoka" Amesema Zawadi
Elia Stephano mwanafunzi wa shule ya msingi Oldonyosambu, ameweka wazi kuwa uwepo wa shule karibu na nyumbani, utasaidia watoto wote kupata elimu kwa kuwa baadhi ya watoto hukosa fursa ya kupata elimu kwa kisingizio cha umabali wa shule.
"Tunamshukuru sana mama, watoto wote wa kijiji cha Lemanda sasa watasoma, wengi walikuwa wanashindwa kupata elimu kutokana na umbali wa shule ilipo" Amebainisha Stephano
Hata hivyo wazazi na walezi wa kijiji cha Lemanda, hawajasita kuishukuru Serikali ya awmau ya sita chini ya uongizi wa Rais Samia kwa ujenzi wa shule hiyo ya msingi.
Kiongozi wa mila, Laigwanai Olais Sarayan, amempongeza mama Samia kwa mradi huo wenye manufaa kwa watoto wao, na kubainisha kuwa wao kama wananchi wasingeweza kujenga shule hiyo hata kwa miaka mia moja ijayo uongozi wake" Amefafanua Mzee Sarayani
Naye mzee Lukumai licha ya kupongeza juhudi hizo za serikali ya awamu ya sita, amekiri kushirikiana na serikali kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa kwa wakati kwa kuwa tayari tuna madarasa ya awali.
"Sisi kama wazazi tutahakikisha watoto wote wanaanza shule kwa wakati, kuanzia darasa la awali, tutawahudumia watoto wetu kwa chakula, mavali na mahitaji yote ya shule, tumefurahi sana kujengewa shule kijiji chetu cha Lemanda.
Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 306.9 za ujenzi wa shule mpya ya msingi kupitia fedha za mraci wa BOOST zikijumuisha jumla ya madarsa 9, mawili ya elimu ya awali, saba ya elimu ya msingi jengo la Utawala, matundu ya vyoo pamoja na samani za shule hiyo.
ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA
#kaziiendelee
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.