• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Arusha Dc watakiwa kutambua umuhimu wa kulipa ushuru na kodi elekezi

Posted on: February 21st, 2018

Wananchi wakazi wa halmashauri ya Arusha wametakiwa kutambua umuhimu wa kulipa ushuru na kodi  elekezi na kufahamu kuwa mapato hayo hutumika kwenye shughuli za maendeleo katika maeneo yao na taifa kwa ujumla.
Rai hiyo imetolewa na wajumbe wa baraza la madiwani wakati wa mkutano wa baraza hilo wa kujadili taarifa za maendeleo kwa kipindi cha robo ya pili uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa halmashauri hiyo.
Madiwani hao wametoa rai hiyo wakati wa kujadili agenda ya kupitisha mapendekezo ya sheria ndogo za ushuru wa halmashauri hiyo kwa lengo la kukusanya mapato ya ndani agenda iliyokuwa na mijadala yenye mivutano mingi.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Mheshimiwa Noah Lembris amesema kuwa ifike wakati kila mwananchi  kutambua umuhimu wa kulipa kadi na ushuru na kutambua kodi hizo hukusanywa kwa ajili ya maendeleo ndani  ya halmashauri yao.
Ameongeza kuwa halmashauri inaendeshwa kwa mapato ya ndani yanayotokana na kodi na ushuru unaotozwa kwa wananchi na kuongeza kuwa asilimia sitini ya mapato hayo yanarudi kwenye kata na vijiji kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.
" Kodi na ushuru unaokusanywa kwenye maduka, masoko na maeneo mbalimbali zinatumika kuendesha halmashauri na asilimia sitini inarudi vijijini kutekeleza shughuli na miradi ya maendeleo kwa faida ya wananchi wenyewe hivyo ni vema wananchi kulipa bila kukwepa" amesema Mwenyekiti Lembris
  Naye Diwani wa kata ya Musa Mheshimiwa Florah Zelothe amesema kuwa hakuna namna halmashauri inaweza kuendeshwa bila kuwa na mapato hivyo ni vema waheshimiwa madiwani kuwaelimisha wananchi kuwa na tabia ya kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo katika maeneo yao.
Awali Madiwani hao katika mkutano huo licha ya kupitia mapendekezo ya Sheria hizo za Ushuru wamejadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa kipindi cha miezi mitatu na kuweka mipango mikakati ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa robo ijayo ya tatu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.