• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI  KIJIJI CHA BWAWANI WAMASHUKURU MAMA SAMIA KUJENGA SHULE SHIKIZI OLMAPINU

Posted on: November 18th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wananchi hususani watoto na wazazi wa Kijiji cha Bwawani na vitongoji vyake, kata ya Bwawani halmashauri ya Arusha, wailaya ya Arumeru, wamemshukuru mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea madarasa kwenye shule ya Msingi shikizi ya  Olokii katika kitongoji cha Olmapinuu.

Wananchi hao, wamefikia hatua hiyo mara baada ya serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 101 kwa awamu mbili za ujenzi wa miundombinu ya shule shikizi,  ikiwemo vyumba 2 vya madarasa, matundu 10 ya vyoo na nyumba ya mwalimu na tayari wanafunzi wanaendelea na masomo shuleni hapo.

Mkuu wa Idara ya Mipango, halmashauri ya Arusha, Anna Urio, amefafanua kuwa, fedha hizo zimekuja kwa awamu mbili, mishoni mwa mwaka 2021 serikali ilitoa  milioni 40 fedha za  UVIKO 19, zilitumika kujenga vyumba 2 vya madarasa na madawati 25 na mwaka 2022 ikitoa shilingi milioni 61, milioni 50 za ujenzi wa nyumba ya walimu na milioni 11 za ujenzi wa matundu 10 ya vyoo vya wanafunzi.

Aidha katika utekelezaji wa ujenzi wa nyumba ya mwalimu, wananchi wa kijiji cha Bwawani wamejikuta wakisukumwa kuongeza nguvu kazi katika utekelezaji wa miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa watoto na walimu wao.

Wakizungumza na mwandishi wetu, wananchi waliokuwa wakisaidia mafundi kujenga nyumba ya mwalimu, wamebainisha kuwa wamefikia hatua hiyo, kutokana na kuona umuhimu wa nyumba hiyo ya walimu, nyumba ambayo walimu wataishi hapo na kuwafundisha watoto wao.

Mjumbe wa kamati ya Mapokezi ya Ujenzi, Shaban Rashid amesema kuwa, watoto wao wamekuwa wakiteseka kwa miaka mingi, kutokana na shule ya msingi kuwa mbali na kutenganishwa na korongo ambalo wakati wa mvua watoto hushindwa kuvuka na kukosa masomo kwa zaidi ya miezi 4 mpaka 6 wakati mwingine.

"Tunamshukuru mama Samia, kweli amekikumbuka kijiji chetu hasa kitongoji cha Olmapinuu, kitongoji ambacho watoto wengi waliacha shule kwa kukata tamaa ya umbali na wengine kucheleweshwa kuandikishwa shule kutokana na wazazi kuhofia madhara watakayokutana nanyo njiani hasa kipindi cha mvua". Amefafanua Ally.

Aidha ameipongeza serikali kwa kuwashirikisha wananchi katika usimamizi wa miradi, jambo ambalo linawafanya wananchi, kumiliki miradi lakini linawafanya kujihakikishia matumizi sahihi ya pesa zao za Umma.

Hata hivyo wanafunzi wa shule hiyo shikizi, wameipongeza na kuishukuru serikali na kudai kuwa kwa sasa wanasoma kwenye madarasa mazuri, na watoto wengi wanapata fursa ya kuanza shule kwa wakati.

Yunus Alley mwanafunzi wa darasa la awali, amesema kuwa kwa sasa wanasoma kwa furaha, madarasa ni mazuri, shulemiko karibu na nyumbani.

Akitoa ushuhuda wa kuanza kwa shule hiyo mwalimu Zakayo Lukumai, ameema shule ilianza mwka 200 kwa wanafunzi kukaa chini,na baadaye kupata darasa la nyasi, mwaka 2022 serikali imejenga madarasa mawili mazuri, madarsa ambayo yamesababisha ongezekomla wanafunzi shule hapo.

"Kwa sasa tuna ongezeko la wanafunzi, wamefikia 110, kutoka wanafunzi  40 hapo awali, kwa sasa wazazi wamepata mwamko wa kuwaandikisha watoto kuanza shule". Amesisitiza  Mw. Lukumai

Awali Serikali inandelea na mkakati wa kuboresha miundo mbinu ya shule ili kuhakikisha watoto wenye umri wa kwenda shule, wanaandikishwa kwa wakati.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍


PICHA ZA WANAFUNZI WAKIWA DARASANI NA MAENDELEO YA UJEZNI WA NYUMBA YA MWALIMU NA VYOO 


Wanafunzi wa darasa la kwanza shule shikizi ya Olokii kitongoji cha Olmapinuu kijiji cha Bwawani, wakifurahia masomo baada ya serikali kujenga mdarasa mazuri shukeni hapo.




Wananchi wakisaidia mafundi ujenzi wa nyumba ya mwalimu

,




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.