• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI OLMRINGARINGA WAIOMBA KUBADISHA MATUMIZI YA ARDHI ENEO LILILOKUWA LIKITUMIWA KAMA JOSHO

Posted on: February 5th, 2022

Elinipa Lupembe.

Wananchi wa kijiji cha Olimringaringa kata ya Kimnyaki, halmashauri ya Arusha, wameiomba serikali kubadilisha matumizi ya ardhi, katika eneo la serikali lililokuwa likitumika kama josho la kuoshea mifugo kijijini hapo, badala yake, eneo hilo litumike kujenga Kituo cha afya.

Wananchi hao wametoa rai hiyo, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa halmashauri hiyo, wakati wakiwa kwenye ziara kukagua miradi ya maendeleo na maeneo ya umma kijijini hapo.Wananchi hao wameweka wazi kuwa, historia ya eneo hilo, lilikuwa likitumiwa na wafugaji kuogeshea mifugo yao, lakini kwa miaka mingi sasa eneo hilo halitumiki, kutoka na wafugaji wengi sasa, kuhamia kwenye ufugaji wa kisasa, wa kifuga ndani, ambapo kila mfugaji humudu kuosha mifugo yake nyumbani.

Wamethibitisha kuwa, josho hilo kwa muda mrefu sasa halitumiki, wao kama wanakijiji wameendelea kulitunza eneo hilio kwa muda mrefu, na kuongeza kuwa, imefika wakati wanaomba kubadilisha matumizi, ili eneo hilo liweze  kutumika kwa shughuli nyingine za kijamii, kuliko kubaki bila kutumika kwa muda mrefu.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Olimringaringa Mheshimiwa, Wilson Emanuel, aliuomba uongozi wa halmashauri kufanya ukarabati wa  josho hilo, lakini baadhi ya wananchi walipinga hoja hiyo na kuomba eneo hilo, kujengwa kituo cha afya, kutoka na ukweli kwamba kwa sasa wafugaji wengi wamebadilisha mfumo wa ufuagi ambao, kila mfugaji humudu kuhudumia mifugo yao nyumbani, tifauti na hapo awali.

Naye Eliakim Kilusu, mkazi wa kijiji cha Olmringaringa, amethibitisha kuwa kata ya Kimnyaki haina Kituo cha afya na wananchi wa eneo hilo, hulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya, na kusisitiza kuwa, ni vema eneo hilo likabadlishwa matumizi na kujenga kituo cha afya.

"Kipaumbele chetu kwa sasa ni kuwa na kituo cha afya katika eneo hili, kwa kuwa hatuna zahanati, watu wanapata shida na kutumia gharama kubwa, pindi wanapougua hasa nyakati za usiku, kufuata huduma za afya vijiji vya jirani, ambapo kuna umbali mrefu" amesisitiza Kilusu.

Akijibu hoja za wananchi hao, Makamu Mwenyekiti, halmashauri ya Arusha na Diwani wa kata ya Mateves, mheshimiwa Freddy Lukumay, licha ya kuwapongeza wanachi hao kwa kutunza eneo hilo kwa muda mrefu, amewaagiza viongozi wa kijiji hicho, kufanya mkutano wa wananchi wote, ili wakubaliane kile wanachohitaji serikali  yao kufanya katika eneo hilo na kumuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha na timu yake ya watalaamu, kusimamia ombi la maamuzi yatakayoletwa na wananchi hao wa Kimnyaki.

Naye Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, ameahidi kutegeleza agizo hilo kwa kuzingatia matakwa na maamuzi yatakayofanywa na wanachi hao wa Kimnyaki,  kupitia vikao na mkutano wa kisheria na kuliwasilisha ofisini kwake.

"Niwapongeze pia kwa kutunza eneo hili, na sio kulitunza tu, zaidi kwa kuwa na hati miliki ya kimila, jambo ambalo vijiji vingi vinamiliki maeneo bila kuwa na hati, fanyeni maamuzi ya nini mnahitaji kwa kuzingatia kipaumbele cha huduma mnayohitaji, pamoja na kufuata taratibu za vikao na mkutano wa kisheria, halmashauri na timu ya watalamu tutafanyia kazi maamuzi yenu kwa wakati na kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu" . Amesisitiza Msumi

Awali wajumbe hao wa Kamati ya Fedha, wamefanikiwa kutembelea miradi 9 ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na eneo hilo la wazi linalomilikiwa na serikali kupitia Idara ya mifugo lililoko kijiji cha Olmringaringa kata ya Kimnyaki.

ARUSHA DC 

KaziInaendelea✍✍✍




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.